WATU WATANO WAMEKUFA BAADA YA KUCHOMWA MOTO NA WANANCHI WENYE HASIRA

Watu watano wamekufa kwa kuchomwa moto na wananchi wenye hasira kali kwa tuhuma za kuiba rambirambi ya shilingi elfu 65.

Tukio hilo limetokea mchana huu majira ya saa saba na nusu katika kitongoji cha Nyantolotolo A nje kidogo ya mji wa Geita.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa Mzee Luhemeja alifiwa na mjuukuu wake na baada ya kuisha msiba huo hapo jana watu wote walisambaa wakiwepo pia watuhumiwa waliouawa hao na kurudi makwao.

Mashuhuda wameongeza kuwa usiku huo watu wanaosadikiwa wanaodaiwa kuwa 8 walifika Nyunbani kwa mzee huyo na kuingia ndani ambapo walimkuta mtoto mdogo na kumpiga kofi baadae wakamfuata mzee wakampiga na kumuonba awapatie fedha kwa usalama wake.

Baada ya kumpiga mzee huyo walifanikiwa kuchukua shilingi elfu 60 zinazodaiwa kuwa ni pesa za rambirambi zilizotolewa wakati wa msiba baada ya mzee huyo na kufiwa na mjukuu wake.

Imeelezwa kuwa baada ya kuchukua pesa kwa mzee watuhumiwa hao na kumfata mke wake ambaye jina lake halijafahamika naye wakampiga na kumuumiza kisha kuchukua kiasi cha shilingi elfu 5 kisha wakatokomea kusikojulikana.

Baada taarifa kusambaa kuwa kuna uvamizi umetokea jeshi la jadi sungusungu lilianza msako na kufanikiwa kumkamata mmoja wa watuhumiwa akiwa na damu kwenye nguo zake na kumhoji juu ya tukiohilo, mtuhumiwa aliwataja wenzake mmoja baada ya mwingine na jeshi hilo kuwatia mbaroni wote watano.

Baada ya watuhumiwa kutiwa mbaroni wananchi wenye hasira kali walianza kuwashushia kipigo kisha kuwachoma moto hapo hapo huku mmoja kati ya hao watano akikatwa panga kwenye mguu nakudumbukizwa kwenye kisima na kufia humo humo.

Mganga mfawidhi wa Hospitali ya wilaya Geita Dkt Adam Sijaona amekiri kupokea miili ya marehemu majira ya saa nane na nusu mchana wa leo na gari la polisi waliofika muda mfupi baada ya tukio wakiwa na kamanda wa polisi wa mkoa wa Geita.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoawa Geita kamishina msaidizi mwandamizi Leonard Paul amethibitisha kutokea kwa tukio na kuwataja majina yao kuwa ni Juma Patrick Kigara,Marwa,Chacha Kigara, na wawili waliofahamika kwa Eze na Shija na wa tano akiwa hajafahamika jina lake.

Kamanda Paulo amesema tayari watu watatu akiwemo kiongozi wa jeshi la jadi wanashikiliwa na polisi kwa mahojiano zaidi huku jeshi likiendelea kufanya uchunguzi zaidi kuhusiana na tukiohilo.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mwandishi wa habari hizi kutoka mkoani Geita Valence Robert asilimia kubwa ya wanaumme wamekimbia miji yao kutokana na msako mkali unaofanywa na jeshi la polisi kubaini wahusika wa tukio hilo.