ACHEZEA KICHAPO MKAPA KUFA BAADA YA KUKUTWA UCHI KWENYE MACHIMBO YA DHAHABU

Mtu mmoja Yunge Maboja (70) Mkazi wa Kijiji cha Kapanda Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi amefariki dunia baada ya kushambuliwa na wananchi kwa kupigwa na silaha za jadi ngumi na mateke baada ya kukutwa uchini usiku wa manane kwenye shimo la kuchimba dhahabu na kutuhumiwa kuwa alikuwa akiroga ili mwenye shimo hilo asipate madini ya dhahabu Kwa mijibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Kamishina Dhahili Kidavashari alisema tukio hilo la kushambuliwa kwa mtu huyo lilitokea hapo juzi majira ya saa saba usiku katika kijiji hicho cha Kapanda Alisema wiki tatu kabla ya tukio hilo marehemu alimuazimisha Idd Kipara shoka ambalo alikuwa akilitumia katika shughuli zake ulinzi katika shimo la kuchimba madini aina ya dhahabu la Juma Ngegeshi.

Alieleza marehemu alianza kumtafuta mtu aliye muazimisha shoka na ndipo siku hiyo ya tukio majira ya saa saba usiku alipofika kwenye shimo la kuchimba dhahabu la mtu mmoja aliyejulikana kwa jina moja La Abui ambapo alichungulia ndani ya shimo ambalo ndani yake walikuwemo watu wili wakifanya shughuli hizo za uchimbaji wa madini Kamanda Kidavashari alisema watu hao waliokuwa ndani ya shimo walishitushwa na kitendo cha marehemu kuwachungulia mida hiyo ya usiku wa manane wakiwa ndani ya shimo hivyo iliwalazimu watoke nje ya shimo hilo la kuchimba madini ya dhahabu ndipo walipotoka na kumkuta marehemu akiwa uchi.

Alisema ndipo watu hao wawili Abui na Hassan walipoanza kumshambulia marehemu kwa kashfa za kuwa marehemu kuwa ni mchawi na ndio maana amefika kwenye shimo lao akiwauchi na ndio maana wamekuwa hawapati madini ya dhahabu kwenye shimo hilo kwa muda mrefu.

Kidavashari alieleza ndipo walipoamua kumkamata huku akiwa uchi na kuanza kumshambulia kwa fimbo na mateke na kumlazimisha awapeleke kwa mwenyeji wake Juma Ngegeshi ili awapatie uchawi ambao ulikua umebaki atowe uchawi uliobaki nyumbani kwake.

Walipofika nyumbani kwa Juma Ngegeshi walimkuta mkewe aitwaye Asha Shaban ambae baada ya kuwafungulia mlango walimtaka awaonyeshe uchawi ilikuwa umebaki ndani ya nyumba hiyo na Asha aliwajibu ndani ya nyumba yake hakuna kitu kama hicho na hafamu kitu kama hicho na kisha alianza nae kushambuliwa kwa fimbo usoni na mgongoni.

Alieleza hari hiyo ilimfanya Asha apige mayowe ya kuomba msaada na ndipo majirani walipofika hapo na kukuta marehemu yuko uchi nao waliungana kuaanza kumshambulia yeye pamoja na Asha hari ambayo ilimfanya Asha ajifungie ndani ya nyumba yake.

Kidavashari alieleza majeruhi wote wawili walifikishwa kituo cha polisi cha Mpanda na kisha walipelekwa Hospitali ya Wilaya ya Mpanda na marehemu alilazwa kutokana na hari yake kuwa mbaya na arifariki dunia akiwa anaendelea kupatiwa matibabu.

Jitihada za kuwasaka wahusika wa tukio zilifanyika ambapo watu wawili wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano ambao ni Yunge Hassan 43 mkazi wa Mtaa ya Kashaulili na Ayub Samwel 30 Mkazi wa Kijiji cha Kapanda na wengine wamekimbia.

Chanzo: Katavi yetu