TABU LEY AZIKWA KINSHASA

Shughuli ya mazishi ya marehemu Tabu Ley Rochereau gwiji wa Rumba Afrika, inaendelea mjini Kinshasa, DRC.

Viongozi wa serikali ya DRC wamehudhuria mazishi hayo huku waakilishi kutoka nchi jirani ya Congo Brazaville pia wamehudhuria mazishi hayo.

Tabu Ley alifariki mwezi Novemba akiwa na umri wa miaka 76 akipokea matibabu nchini Ubelgiji.

Tabu Ley alikiri rasmi kwamba ana watoto 49.

Lakini mwandishi wa BBC katika mazishi hayo anasema kuwa zaidi ya watu 80 wamejitokeza na kusema kuwa baba yao nimwanamuziki huyo na kwamba wengi waowanataka kuzungumza katika sherehe hiyo.

Tabu ley aliyejulikana kama mfalme wa muziki wa rumba aliaga dunia mwezi uliopita mjini Brussels ,ubelgiji akiwa na miaka sabini.

Wengi walimkumbuka Tabu Ley kwa mziki wake na kwa talanta yake kwa utunzi wa nyimbo zake zilizowagusa watu wengi Afrika. Tabu Ley amefanyiwa mazishi ya kitaifa Mwanamziki huyo ambaye pia alikuwa mwanasiasa, hakuwahi kupona tangu alipougua kiharusi mwaka 2008 na hali yake iliendelea kuwa mbaya hadi alipofariki Novemba 30.

Alizaliwa mwaka 1937 katika kijiji kimoja kidogo Magharibi mwa mkoa wa Bandundu, na hapo ndipo nyota yake ilianza kung'aa a katika fani ya muziki wa Rumba mapema miaka ya sitini.

Baadhi ya nyimbo alizoimba zilikuwa Adios Thethe na Mokolo nakokufa, na zilisaidia katika kufanya mziki wa Rumba kupendwa sana.

Tabu Lei alitaka sana kuwa waziri wa utamaduni katika serikali ya Laurent-DesireKabila --babake rais Joseph Kabila, lakini badala yake akawa naibu gavana wa mji waKinshasa.

Alikimbilia usalama wake wakati wa utawala wa aliyekuwa rais Mobutu Sese Seko kati ya mwaka 1965 to 1997, na mnamo mwaka 1990, serikali ya Mobutu ikapiga marufu album yake Trop, c'est trop.