WANAJESHI WA MAREKANI WAACHIWA LIBYA

Makao Makuu ya Ulinzi nchini Marekani, Pentagon imesema wanajeshi wake wanne waliokuwa wakishikiliwa kwa saa kadhaa nchini Libya wameachiwa.

Wanajeshi hao wanne waliripotiwa kukamatwa wakati alipokuwa wakiangalia nji za kuwaondoa wafanyakazi wa Ubalozi wa nchi hiyo nchini Libya.

Walikamatwa katika katika kituo cha uchunguzi wa magari karibu na Sabratha, mashariki mwa mji mkuu wa Tripoli. Na baadae walikabidhi kwenye wizara ya mambo ya ndani.

Wanajeshi hao wanne wanasemekana walikuwa wamebeba silaha, na moja kati ya magari yao yanaripotiwa kuchomwa moto.

Picha za wanajeshi hao wakionyesha hati mbili za kusafiria pamoja na vitambulisho zilichapishwa kwenye mitandao ya kijamii.

Maafisa Ubalozi wa Marekani walikuwa wakifanya kazi zao nchini Libya chini ya ulinzi mkali baada ya shambulio la mwaka jana kwenye kikosi cha Umoja wa Mataifa eneo la Benghazi ambalo lilisababisha kifo cha Balozi wa Marekani nchi Libya.