WANAJESHI WAWILI WA UFARANSA WAUWAWA AFRIKA YA KATI

Wanajeshi wawili wa Ufaransa wameuawa katika mapigano katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Rais wa Ufaransa Francois Hollande"amepokea taarifa hiyo kwa masikitiko makubwa" kwamba askari hao waliuawa usiku mjini Bangui.

Hivyo ni vifo vya kwanza kwa askari wa Ufaransa kuuawa tangu Ufaransa itume askari wake 1,600 nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati wiki iliyopita wakiwa katika operesheni ya kijeshi inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa.

Jamhuri ya Afrika ya Kati imekuwa katika ghasia tangu kiongozi wa waasi Michel Djotodia amtimue madarakani Rais Francois Bozize mwezi Machi mwaka huu.Akajitangazia madaraka kama kiongozi wa kwanza wa Kiislam nchini humo ambao idadi kubwa ya wananchi ni Wakristo na hivyo kuchochea umwagaji damu kwa miezi kadhaa kati ya wapiganaji wa Kiislam na Wakristo.

Spika wa bunge la Ufaransa Claude Bartolone, amewaambia waandishi wa habari kwamba askari hao wa kikosi cha anga walipata ajali ya ndege karibu na uwanja wa Bangui.

"Walijeruhiwa na haraka kupelekwa kituo cha upasuaji, lakini kwa bahati mbaya walipoteza maisha," amesema.

Taarifa kutoka ofisi ya Rais Hollande imesema askari hao walipoteza maisha yaoili kulinda maisha ya watu wengine".

"Rais ameelezea shukrani zake kwa askari hao wawili waliojitolea maisha yao na ameelezea imani yake kamili kwa vikosi vya Ufaransa vilivyoko nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati ya kulinda amani nchini humo, katika kuwalinda watu na kuhakikisha misaada ya kibinadamu," taarifa hiyo imesema.

Mapigano kati ya Wakristo na waasi wa Kiislam wa Seleka yamesababisha vifo vya watu wengi.

Kundi la Wakristo walishambulia msikiti mjini Bangui Jumanne.

Rais Hollande amehudhuria ibada ya kumwombea marehemu Nelson Mandela, nchini Afrika Kusini na anatarajiwa baadaye Jumanne kuelekea mjini Bangui, Jamhuri yaAfrika ya Kati.

Mwandishi wa BBC,Thomas Fessy katika mjiwa kaskazini wa Bossangoa amesema vikosivya Ufaransa, pamoja na vile vya kulinda amani vya Afrika - Jumatatu, walifanya operesheni ya kuwapokonya silaha wanamgambo na wapiganaji wa Kiislam ambao wanadai wawe sehemu ya jeshi jipya la taifa la nchi hiyo.

Hali ya wasiwasi imebakia nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, amesema mwandishi wetu.

Vikosi zaidi vya jeshi kutoka Ufaransa viliongezwa Ijumaa baada ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuunga mkono azimio la kurejesha utulivu kwa"njia zozote zinazowezekana".

Chama cha Msalaba Mwekundu, kimesema watu 394 walkiuawa katika siku tatu za mapigano mjini Bangui. Wengi wao wakiwani watoto.

Jeshi la Ufaransa limesema limefanikiwa kurejesha hali ya utulivu katika baadhi ya maeneo mjini Bangui kufikia Jumatatu usiku.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon amesema askari wa kulinda amaniwapatao 9,000 watahitajika nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, na ana matumaini kuwa hatimaye watakuwa sehemu ya operesheniya Umoja wa Mataifa.

Inakadiriwa kuwa asilimia 10% ya watu milioni 4.6 nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati wameyakimbia makaazi yao, wakati ambapo zaidi ya milioni moja wanahitaji msaada wa dharura wa chakula, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.