KIONGOZI WA MUSLIM BROTHERHOOD AFIKISHWA MAHAKAMANI

Kiongozi wa vuguvugu la Muslim Brotherhood, amefikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza tangu kukamatwa kwake.

Hata hivyo mahakama imeahirisha kesi hiyo hadi Februari 11 mwaka 2014,Wadadisi wanasema ni sehemu ya kampeini ya serikali dhidi ya vuguvugu hilobaada ya jeshi kumuondoa mamlakani aliyekuwa rais Mohamed Morsi.Mohamed Badie -- aliyefikishwa mahakamani na viongozi wengine wa kundi hilo, alikanusha madai kua alitumia kundi hilo kuchochea ghasia.

Miongoni mwa washitakiwa wenza wa Badie ni pamoja na Isam al-Iryan, Muhammad al-Biltaji, Basim Udah na Safwat Hijazi. Makosa mengine wanayokabiliwa nayo ni pamoja na kuundagenge la kuwahangaisha watu, uharibifu wamali ya watu binafsi na kumiliki silaha kinyune na sheria.

Makosa wanayokabiliwa nayo yanatokana na ghasia za mwezi Julai ambapo makabiliano yalizuka kati ya wafuasi elfu tano wa Mohammed Morsi pamoja na majeshi katika eneo la Giza na katika msikitiwa Al-Istiqamah baada ya kungo'olewa mamlakani kwa Mohammed Morsi.

Hata hivyo Badie Alihoji kwa nini uchunguzi haukufanyika kuhusu kifo cha mwanawe pamoja na kuteketezwa kwa makao makuuya Brotherhood.

Wanafunzi katika chuo kikuu cha Al Azhar wameendelea kuandamana na kulazimisha polisi kuingia chuoni humo ili kusitisha vurugu zao.