WATU 29 WAJERUHIWA KATIKA AJALI MBILI TOFAUTI

Watu 29 wamejeruhiwa baada ya kutokea kwa ajali mbili tofauti katika eneo la Mikese na Mkambalani, barabara kuu ya Morogoro-Dar es salaam, moja ikihusisha basi la Nganga likitokea Dar es salaam kuelekea Mbeya na basi la Sumry likitokea Tunduma ambalo limegongana uso kwa uso na coster likijaribu kulipita gari jingine lililokuwa mbele.

ITV imefika eneo la tukio na kushuhudia ajali hizo, ambapo ajali ya kwanza imetokea majira ya saa 2 usiku katika eneo la Mkambalani, ikihusisha basi la kampuni ya Sumry likitokea tunduma kwenda Dar es salaam ambalo limegongana uso kwa uso na bas dogo la abiria aina ya costa lililokuwa likitokea dar es salaam kuelekea mbeya na kusababisha majeruhi 15, na chanzo cha ajali kikidaiwa ni dereva wa sumry kujaribu kulipita gari lililokuwa mbele, na kukutana uso kwa uso na costa, huku ,ajali ya basi la nganga ikitokea majira ya saa 3 na nusu asubuhi, katika eneo la miembeni mikese, baada ya kupata pancha kwa tairi ya mbele kulia na kusababisha majeruhi 14 na majeruhi hao wamepelekwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro kwa matibabu.

Aidha mashuhuda wa ajali hiyo waliokutwa eneo la tukio nao wamezungumza kuhusiana na ajali hizo.

Mganga wa zamu katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro, Dk Alex Makala, amesema majeruhi wengine wametibiwa na kuruhusiwa na kwamba wamebaki majeruhi 14 wakiwemo 12 wa Sumry na wawili wa Nganga, na wengi wamepata majeraha madogo madogo na wanaendelea vyema na matibabu, huku kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro faustine shilogile akizungumza kwa njia ya simu, amesema dereva wa basi la sumry mhina mohamed(39) mkazi wa mbeya amejisalimisha polisi majira ya asubuhi baada ya kukimbia kufuatia ajali hiyo, huku dereva wa basi la Nganga Alex Elia(49) mkazi wa Misufini Morogoro akiishikiliwa kwa mahojiano zaidi.

Chanzo: ITV