WATOTO SITA WAUWAWA BENGHAZI

Watoto sita wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa nchini Libya baada ya shule yao mjini Benghazi kushambuliwa kwa guruneti.

Maafisa wanasema kuwa gureti hilo lilitupwa mahala watoto hao walipokuwa wakicheza katika shule binafsi eneo la Tabilinu wakati wa mapumziko.

Mji wa Benghazi, umeshuhudia, misururu ya mashambulizi katika mwaka mmoja uliopita, lakini mashambulizi dhidi ya shule sio rahisi kutokea.

Haijulikani nani aliyehusika na shambulizi hilo.

Mkazi mmoja wa Mji wa Benghazi, ameambia BBC kuwa aliona mtu mmoja akitengeza guruneti kwa mdomo wake tayarikwa mashambulizi.

Kisha akaitupa guruneti hiyo shuleni humo kabla ya kutoroka kwa gari moja dogo.

Watu walionekana wakikimbilia usalama wao baada ya shambulizi hilo.

Shambulizi lenyewe lilifanyika kabla ya saa tano asubuhi watoto walipokuwa nje wakicheza.

Afisaa mmoja wa usalama amesema kuwa shambulizi halikuwa na nguvu kubwa, na kuwa polisi wameanza kuwasaka washukiwa.

Mji wa Benghazi ulikuwa kitovu cha harakati za mapinduzi ya kiraia mwaka 2011 ambayo yalimuondoa mamlakani hayati Muammar Gaddafi.

Tangu hapo, mji huo umekuwa ukikumbwa na mashambulizi ya mara kwa mara dhidi ya taasisi za serikali.