WACHIMBAJI 17 WAKWAMA MGODINI

Vikosi vya uokozi vimeingia katika mgodi wa dhahabu nchini Afrika Kusini kujaribu kuwaokoa wafanyakazi 17 wa kuchimba mgodi waliokwama mgodini baada ya moto kuzuka.

Kampuni hiyo ya madini Harmony Gold,inasema kuwa moshi uliofuka pomoja na mawe yaliyokuwa yanaanguka yanasemekana kutatiza shughuli ya uokozi.

Kampuni hiyo inasema kuwa imeweza kuwasiliana na wachimba migodi walionaswa.

Kadhalika imesema kuwa imeweza kuwasiliana na wafanyakazi wengine 8 walioweza kujiokoa kutokana na moto uliozuka Jumanne usiku na kutafuta hifadhi katika kituo kimoja kilicho umbali wa mita 1700 chini ya ardhi.

Wachimba migodi tisa bado hawajulikani waliko.