TUTU AMSIHI MUSEVENI

Askofu mstaafu wa Cape Town, Desmond Tutu, amemsihi Rais Museveni wa Uganda asitie saini mswada ulioleta utatanishi kuhusu wapenzi wa jinsia moja.

Askofu Tutu, aliyewahi kupata tuzoya amani ya Nobel, alisema amevunjika moyo kuwa Rais Yoweri Museveni anaonesha kubadilisha msimamo wake, kwa vile awali alisema kuwa hata ruhusu mswada huo kuwa sheria.

Desmond Tutu alisema haistahikikuwa na ubaguzi kama huo, na alitoa mifano ya mfumo wa zamani wa ubaguzi wa rangi uliokuwako Afrika Kusini na ubaguzi wa Wa-Nazi wa Ujerumani.

Alisema hiyo ni mifano mibaya kabisa.

Awali mswada wa Uganda ulipendekeza kifo kwa vitendo vya kulawiti na baadae kubadilishwa kuwa adhabu ya kifungo.