NYOKA WAVULUGA SHUGHULI ZA MAHAKAMA

CHANGAMOTO nyingi za muda mrefu zinazoikabili idara ya mahakama katika wilaya ya Ukerewe, Mwanza sasa zimechukua sura mpya kwa baadhi ya shughuri za mahakama kuvulugwa na Nyoka.

Maelezo ya tukio hilo la aina yake lililoshutua wengi yameelezwa katika siku ya sheria ambayo kiwilaya ilifanyika katika uwanja wa mahakama ya wilaya hiyo mjini Nansio.

Akizungumzia changamoto zinazoikabili idara ya mahakama hakimu mkazi wa mahakama ya mwanzo Bukonyo Malisel Ndimila alisema hali ya uchakavu wa majengo ya mahakama zote katika wilaya hiyo inatisha.

Akifafanua alisema mbali ya changamoto nyingine ikiwemo watumishi wa idara hiyo kutokuwa na nyumba na nyezo za usafiri lakini majengo ya mahakama hasa jengo la mahakama ya mwanzo Bukonyo sasa limegeuka pango la Popo na makazi ya Nyoka.

Katika maelezo yake zaidi Ndimila alikwenda mbali zaidi na kueleza kuwa tangu apelekwe katika mahakama hiyo hapo mwaka jana hadi sasa amenusulika kuumwa na nyoka katika matukio matano tofauti.

Alisema katika matukio hayo Nyoka hao utokea juu ya daliya jengo la mahakama hiyo na uanguka chini wakati mwingine shughuri za mahakama zikiendelea na kusababisha mtafaluku mkubwa.

Akithibitisha tatizo hilo hakimu mkazi mfawidhi wa wilaya hiyo Faustin Kishenyi alisema mbali ya hali mbaya ya uchakavu wa majengo ya mahakama pia watumishi wote wakiwemo mahakimu wote wanne pamoja na yeye awana nyumba.

Nae Luhasha Rouben aliyekuwa hakimu wa wilaya hiyo kabla ya kustahafu hapo mwaka jana alisema changamoto hizo zinatokana na idara hiyo kutengewa bajeti kidogo isiyokidhi maitaji.

Alisema taarifa zilizopo zinaonyesha kuanzia bajeti ya miaka miwili iliyopita kuludi nyuma idara ya mahakama kwa nchi nzima utengewa fedha isiyozidi bil. 17 kwa mwaka lakini fedha inayopelekwa uwa chini ya kiasi kilichotengwa.

Katika maelezo yake zaidi Luhasha alisema katika mwaka wa fedha wa 2013/014 idara hiyo kwa nchi nzima ilitengewa sh. Bil 42 lakini hadi sasa fedha iliyotolewa ni sh. Bil. 5.5 na kuzitaka mamlaka za juu kuwana mtizamo mpya dhidi ya idara hiyo vinginevyo matatizo yataendelea kubaki kama yalivyo.

Mkuu wa wilaya hiyo Mery Tesha akizungumza baada ya kupokea maelezo hayo amekili kuwa matataizo hayo yanatokana na ufinyu wa bajeti na kutaka wadau mbali mbali kushiliki kutatua.

Hata hivyo alisema serikali anatambua umuimu wa idara hiyo na kuongeza kuwa wakati inakamilisha ujenzi wa mahakama ya mwanzo na kituo cha polisi kwa gharama ya sh. Mil. 250 katika kisiwa cha Ilugwa pia imetenga sh. Mil. 120 kwaajili ya ujenzi wa mahakama ya mwanzo katika kisiwa cha Ukara.