MTU MMOJA AFARIKI, 38 WAJERUHIWA

Mtu moja amefariki duni na wengine 38 wamejeruhiwa baada ya basi la Bunda kugonga kichwa cha treni katika makutano ya reli na barabara wilayani Manyoni.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambayo imehusisha basi la Bunda lenye usajili wa namba T 782 BKZ lililokuwa likitokea mkoani Dodoma na kuelekea mkoani Mwanza, mkuu wa wilaya ya Manyoni bi Fatuma Toufiq amesama ajali hiyo imetokea majira ya asubuhi saa mbili tarehe 28 katika makutano ya barabara na reli mjini Manyoni.

Akiongea na ITV na Radio one muuguzi mkuu wa haspitali ya wilaya ya Manyoni Bi. Heliechi Malisa amesema wamepokea maiti moja ambayo imetambulika kwa jina la Perina Bikombo mkazi wa Manyoni na majeruhi thelasini na nane wamelazwa na wanapatiwa matibabu katika hospitali ya wilaya ya Manyoni.


Chanzo:ITV