MUSLIM BROTHERHOOD WASHUTUMIWA KUUNDA JESHI

Utawala nchini Misri, umeishutumu, vugu vugu la Muslim Brotherhood, lililopigwa marufuku kwa kuunda kitengo maalum cha kijeshi Kusini mwa nchi hiyo, ili kufanya mashambulio dhidi ya wanajeshi wa serikali.

Wizara ya usalama wa ndani nchini Misri, imetoa orodha ya majini ya watu kumi na wawili wakitengo hicho, na kuwashutumu kwa kuwauawa maafisa watano wa polisi katika mkoa wa Beni Suef.

Maafisa wa Ulinzi nchini Misri wamewauawa takriban wafuasi elfu moja wa vugu vugu hilo la Muslim Brotherhood, tangua jeshi la nchi hiyo lilipomuondoa madarakani, rais Mohamed MorsiJulai mwaka uliopita.

Kundi hilo limesema kuwa linapinga vikali ghasia na machafuko, lakini kumekuwa na mashambulio kadhaa dhidi ya maafisa wa ulinzi yanayotekelezwa na watu wanaoaminika kuwa wapiganaji wa Kiislamu.

Awali siku ya Jumapili, kiongozi mmoja mwandamizi wa Kiislamu, Abdel Moneim Aboul Fotouh alisema kuwa, taifa la Misri limegeuka na kuwa Jumuhuri la uoga.