NDOA ZA JINSIA MOJA ZAPINGWA UINGEREZA

Maskofu wakuu katika kanisa moja nchini Uingereza wamewaambia viongozi wa dini kwamba hawataruhusiwa kuingia katika ndoa za jinsia moja,na kusema kuwa hawatakubali viongozi wa dini masenge kwenda kinyume na maagizo hayo.

Viongozi wa dini wa kanisa la Ki-Anglikana wanakubaliwa na kanisa hilo kuingia katika uhusiano wa kimapenzi lakini kwamaelewano kwamba hawatashiriki ngono.

Katika mwelekeo wao, maaskofu hao pia wamepiga marufuku maombi yoyote maalum kwa wanadoa wa jinsia moja licha ya ripoti rasmi ya kanisa hilo kupendekeza kwamba viongozi wa dini wanaweza kufanya hivyo iwapo wanajihisi.

Hata hivyo amesema kuwa viongozi wa dini wanapaswa kutoa maombi yasio rasmi kwa wanandoa walio katika uhusiano wa jinsia moja.