BARAZA LA MAWAZIRI LAJIUZULU MISRI

Waziri mkuu wa Misri, Hazem el-Beblawi na baraza lake la mawaziri wamejiuzulu.

Katika taarifa ya moja kwa moja kupitia televisheni, Bwana El-Beblawi alisema kuwa Misri imeshuhudia ongezeko la migomo katika sekta ya umma katika wiki chache zilizopita.

Alisema kuwa hakuna hata serikali moja duniani ambayo inaweza kutimiza mahitaji ya watu wake katika kipindi kifupi sana.

Serikali hiyo ya mpito ilianza kazi mwezi Julai mwaka jana baada ya jeshi kumpindua aliyekuwa Rais Mohammed Mosri.

Taarifa zinasema kuwa uamuzi wabaraza la mawaziri kujiuulu ulitokea baada ya mkutano kati ya mkuu wa majeshi na waziri waulinzi Field Marshal Abdul Fattah al-Sisi.

Inaarifiwa kuwa al-Sisi anatarajiwa kujiuzulu kutoka katika wadhifa wake ili kugombea Urais.