MAPIGANO YAZUKA SUDAN KUSINI

Mapigano yanaripotiwa kuzuka Sudan Kusini kwa mara ya kwanza tangu serikali na waasi kutia saini makubaliano ya kusitisha vita mwezi Januari.

Waasi wanaomtii makamu wa Rais wa zamani Riek Machar, wameshambulia mji wa Malakal, ambao ni mji mkuu wa jimbo la Upper Nile linalozalisha mafuta kwa wingi.

Majeshi ya serikali, yamepambana vikali na waasi hao katika maeneo tofauti ya mji huo.

Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa mjini Juba, (Toby Lanzer), amezitaka pande zote kwenye mzozo huo, kulinda raia.

Makabiliano hayo bila shaka yanazua wasiwasi kuhusu hali ya usalama katika visima vya mafuta Kaskazini mwa nchi.

Mafuta ya Sudan Kusini ndio uti wa mgongo wa uchumi wa nchi hiyo