MKENYA AENDELEA KUSHIKILIWA DAR

Kitengo cha Polisi cha Kupambana na Dawa za Kulevya, kinaendelea kumshikilia raia wa Kenya, Abdulrahman Salim.

Mtuhumiwa huyo anadaiwa kukamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) akiwa na kete 141 za dawa za kulevya aina ya cocaine, hadi jana zilikuwa zimefikia 142.

Salim alikamatwa Januari 31 mwakahuu saa 7:00 usiku akitokeaa nchiniBrazil, kupitia nchini Ethiopia akiwa amepanda ndege ya Shirika la Ethiopia kuja nchini ili aelekee Mombasa nchini Kenya.

Mkuu wa Kitengo cha Kupambana na Dawa za Kulevya, Kamanda Alfred Nzowa alisema mtuhumiwa huyo hadi sasa ametoa kete 142 nakwamba, anaendelea kutoa zingine.

Nzowa alisema walipomhoji mtuhumiwa aliwaeleza kuwa, zilizobaki tumboni zinakadiriwa kuwa tatu hadi tano na inadaiwa idadi hiyo inaweza kuzidi.

"Mpaka sasa tunamshikilia huku tukiendelea kumhoji, inavyoonekana zitazidi idadi aliyotaja mtuhumiwa," alisema Nzowa.

Nzowa alisema kuna baadhi ya watuwa mataifa ya nje wanatumia uwanje wa JNIA kupitisha dawa hizo, wanapokamatwa wanaonekana ni Watanzania wakati siyo kweli.

"Hali hii inachafua taswira ya nchiniyetu, kwa sababu watu wengi wanaokamatwa na dawa za kulevya ni wapita njia kutoka mataifa mengine ikiwamo Kenya, Nigeria na Pakistani," alisema Nzowa.

Tayari, baadhi ya watuhumiwa kutoka mataifa hayo wamekamatwa kwenye uwanja huo.