WALIOBAKWA LIBYA KULIPWA FIDIA

Waziri wa Sheria nchini Libya, salaha al-Marghani, amesema kuwa Baraza la mawaziri limekubaliana kuwa Wanawake waliobakwa wakati wa maandamano na harakati za kuuangusha utawala wa aliyekuwa Rais wa taifa hilo Moammar Gaddafi mwaka 2011 watambuliwe kuwa waathirika wavita.

Amesema makubaliano hayo yanayohitaji kuidhinishwa na Bunge kabla ya kuwa Sheria yatamfanya mwanamke awe sawa na wale wapiganaji waasi waliojeruhiwa halikadhalika watalipwa fidia.

Mahakama ya kimataifa ya uhalifu imekusanya ushahidi kuwa vikosi vya waliokuwa wakimuunga mkono Gaddafi walitekeleza vitendo vya ubakaji kama silaha.

Inaelezwa kuwa Wanawake wanaobakwa mara nyingi wamekuwa wakitengwa nchini Libya, hivyo haijafahamika wanawake wangapi watajitokeza.