WANANCHI WAFUNGA BARABARA

Wananchi zaidi ya 300 kwa mara nyingine wamefunga barabara eneo la Melela wilayani Mvomero wakiishinikiza Serikali kuwaondoa wafugaji ambao wamekuwa wakiingia kwa wingi na kulisha mifugo kwenye mashamba ya wakulima na kuwapiga.

Kufungwa kwa barabara hiyo kwa takribani saa nne kumesababisha magari zaidi ya 400 kukwama eneo hilo la barabara ya Iringa na Morogoro pamoja na kuleta usumbufu mkubwa kwa abiria waliokuwa wakielekea maeneo mbalimbali nchini.

Sasa imekuwa ni mazoea kwa wakazi wa mkoa wa morogoro kutumia njia hii ya kujichukulia hatua ya kufunga barabara pale wanapohitaji kutatuliwa kero zao.

Katika tukio la leo wananchi hao wameamua kufunga barabara mapema asubuhi wakishinikiza serikali ya wilaya hiyo kuwaondoa wafugaji kwa sababu wanalisha mifugo kwenye mashamba yao nakuwapiga wakulima hali iliyopelekea wakulima hao kufunga barabara kwa kuitaka serikali kuingia kati suala hilo.

Naye Mkuu wa Wilaya hiyo ameelezea kuhusu tukio hilo na kuwaomba wanananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi kwani hinaleta madhara kwa wetu wengine ambao hawausiki na mgogoro huo.

Hii ni mara ya 10 kwa kumbukumbu katika kipindi cha miaka miwili iliyopita wananchi wamekuwa wakifunga barabara kwa mawe na magogo pale wanaposhinikiza kutatuliwa kwa kero zao hali ambayo husababisha usumbufu mkubwa kwa watumiaji wa barabara hizo.