MOQTADA AJIUZULU WADHIFA WAKE

Kiongozi wa Dhehebu la Shia nchini Iraq Moqtada al-Sadr ametoa taarifa akitangaza kujiuzulu kwake katika ulingo wa kisiasa.

Katika tangazo ambalo halikutarajiwa na wengi na ambalo liliwekwa katika mtandaowake,Bwana Sadr amesema kuwahatashikilia wadhfa wowote wa serikali wala kuwa na wawakilishi bungeni.

Taarifa hiyo pia imesema kuwa atazifunga afisi zake zote isipokuwa zile za kutoa misaada pekee.

Bwana Sadr na wanamgambo wake wa Mahdi walipata ushawishi nchini Iraq baada ya uvamizi wa marekani nchini humo mnamo mwaka 2003.

Lakini katika miaka ya hivi karibuni amepoteza umaarufu wake kufuatia mzozo kati yake nawaziri mkuu nchini humo Nouri al-Maliki.

Wakati huohuo Aliyekuwa makamu wa rais nchini Iraq amemlaumu waziri mkuu Nouri Al Maliki kwa kusababisha ghasia kati ya wanamgambo wa dhehebu la sunni na vikosi vya serikali ambavyo vinaushikilia mkoa wa Anbar tangu mwezi Disemba.

katika mahojiano na BBC,Tariq al-Hashemi ameishtumu serikali hiyo inayoongozwa na watu wa dhehebu la shia kwa kuzua mgongano huo, kupitia kuwabagua watu wa dhehebu la sunni mbali na kupuuzilia mbali maandamano ya amani.

Bwana Hashemi kwa sasa anaishi kama mkimbizi nchini Uturuki baada ya mahakama moja nchini humo kumpatia hukumu ya kunyongwa kwa madai ya kuendesha magenge ya uhalifu,mashtaka anayoyapinga.

Bwana Hashemi anasema kuwa madai ya serikali ya Iraq kwambauasi huo unaongozwa na vikosi vinavyoshirikiana na kundi la Alqaeda ni njama ya kutotaka kuwajibika mbali na kuvutia hisani kutoka kwa jamii ya kimataifa.