AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA JELA KWA KUMUINGIZIA MTOTO UUME MDOMONI

Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi imemuhukumu Athuman Mussa mwenyeumri wa miaka 54 Mkazi wa Mtaa wa Nsemlwa Mjini hapa kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana na kosa la kumwingizia uume mtoto wa kike mwenye umri wa miaka minne.

Hukumu hiyo ilitolewa hapo jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Chiganga Ntegwa baada ya mahakama kulidhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapona upande wa mashitaka na upande wa mashitaka.

Mshitakiwa alidaiwa kutenda kosa hilo la kumwingizia uume mdomoni mtoto huyo wa kike hapo juni 26 mwaka jana majira ya saa kumi na mbili jioni nyumbani kwake.

Awali katika kesi hiyo mwendesha mashitaka mkaguzi wa polisi Ally Mbwijo alidai mahakamani hapo kuwa siku hiyo ya tukio mshitakiwa alimkuta mtoto huyo akiwa anacheza na watoto wenzake karibu na nyumba yake na ndipo alipomwita mtoto huyo na kuingia nae ndani kwa lengo la kumpa jojo.

Alidai kuwa baada ya mtoto huyo kuingia ndani ya nyumba Athumani alimvutia kwenye kochi sebuleni na kisha alimwingizia uume wake kwenye mdomo wa mtoto huyo hadi hapo alipomaliza haja yake.

Mwendesha mashitaka Ally Mbwijo aliieleza mahakama kuwa baada ya mshitakiwa kumaliza haja yake alimwachia mtoto huyo na ndipo alipotoka mbio na kwenda nyumbani kwao huku akiwa analia.

Aliiambia mahakama baada ya mtoto huyo kufika nyumbani kwao mama wa mtoto huyo alimuuliza analia nini badala ya mtoto kumjibu mama yake mtoto huyo alitema mbegu za kiume ambazo zilikuwa mdomoni mwake na kisha alimwelezea mama yake unyama aliofanyiwa na mshitakiwa.

Alieleza baada ya mama kuelezwa unyama huo aliofanyiwa mtoto wake alianza nae kulia kwa nguvu hari ambayo ilisababisha majirani kufika kwenye eneo hilo na baada ya kuelezwa unyama aliofanyiwa mtoto huyo majirani walikwenda nyumbani kwa mshitakiwa na waliweza kumkamata na kumfikisha kwenye kituo cha polisi.

Hahimu mkazi mfawidhi Chiganga Ntengwa alieleza mahakamani hapo kuwa mahakama baada ya kusikiliza mwenendo mzima wa kesi wa pande zote mbili za mashitakana utetezi mahakama imemwona mshitakiwa amepatikana na hatia hivyo kabla ya mahakama haijatowa adhabu kwa mshitakiwa inatowa nafasi ya mshitakiwa aiombe mahakama kama anasababu za msingi za kuomba apunguziwe adhabu.

Mshitakiwa aliiomba mahakama imwachie huru kwani hakufanya kitendo hicho na zile mbegu za kiume alizotema mtoto huyo zilikuwa ni karanga sio mbegu za kuume.

Mwendesha mashitaka Ally Mbwijo alipinga vikari utetezi huo na kuiomba mahakama itowe adhabu kali kwa mshitakiwa ili iwefundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.

Hakimu mkazi mfawidhi Chiganga Ntengwa baada ya kuzisililiza pande hizo mbili aliieleza mahakama kuwa mshitakiwa amepatikana na hatia ya kifungu cha sheria namba 154 kifungu kidogo cha kwanza a na cha pili suraya 16 cha marekebisho ya mwaka 2009.

Hakimu Chiganga Ntengwa aliiambia mahakama kuwa kutokana na mshitakiwa Athumani Mussa kupatikana na hatia mahakama imemuhukumu kwenda jela kifungo cha maisha.