MCHUNGAJI AHUKUMIWA KWA UBAKAJI

Kiongozi wa kanisa moja nchini Zimbabwe amehukumiwa kifungo cha miaka 40 jela kwa kosa la kuwabaka wanawake watatu na kukutwa na vifaa vya kuchochea kujamiiana.

Kiongozi huyo, Martin Gumbura (57) wa Kanisa la RMG Independent End Time Message alitiwa hatiana katika makosa manne ya ubakaji kwenye mahakama ya mjini Harare. Gumbura ana wake 11 na watoto 30 na aliiambia mahakama kwamba alikuwa akitarajia kupata watoto 100 katika maisha yake.

Wake zake wote walikuwa wakihudhuria mahakamani hapo wakati wa kesi hiyo na walikuwa wakijumuika na watu wengine waliokuwa wakihudhuria makahamani hapo hadi siku hukumu ilipotolewa.

Alihukimiwa kifungo cha mika 50 jela lakini miaka 10 imepungizwa katika adhabu hiyo baada ya kuonyesha tabia njema wakati wa kesi hiyo.

Hukumu nyingine ya kifungo cha miaka minne jela kwa kukutwa na vifaa vya kuchochea kujamiiana itatumikiwa sambamba na hukumu hiyo ya kifungo cha miaka 40. Waendesha mashtaka waliiomba mahakama kwamba Gumburu anatakiwa ahukumiwe kifungo cha miaka 25 jela kwa kila kosa, lakini hakimu alieleza kwamba hana mamlaka ya kutoa hukumu ya kifungo cha muda mrefu namna hiyo.

Hakimu huyo alimwelezea Gumbura kama mbwa mwitu aliyevaa ngozi ya kondoo ambaye amekuwa akiwaghilibu waumini wa Kanisa hilo.

"Mahakama imejaribu kutoa adhabu ambayo itawatendea haki wote, malalmikiwa na walalamikaji.

Mtuhumiwa hutu ni kama mbwa mwitu aliyevaa ngozi ya kondoo," alisema.

"Msingi wa huduma ya Kanisa ni kumwabudu Mungu na si kuzini na mabinti na wanawake na kuwatishia kwamba kwa kutofanya hivyo watapatwa na balaa," aliongeza hakimu huyo.

Alisema ni wajibu wa wachungaji nawasimamizi wa kanisa kujua kuhusumadhila yanayowakumba waumini wao, pia kujua udhalilishaji na unyanyasaji wa kijinsia unaowakumba wanawake na kutafuta namna ya kuukemea.

Awali Gumbura alikuwa akikabilwia na mashtaka tisa ya kuwalaghai na kuwabaka wanawake sita lakini alifutiwa mashtaka manne yaliyowahusisha wanawake watatu kutokana na kukosekana kwa ushahidi wa kutosha.

Hivi karibuni, mtu mwingine mjini Harare alihukumiwa kifungo cha miaka 290 jela kwa kosa la kuwadhalilisha na kuwabaka wanawake 13. Mtu huyo, Thomas Chirembwe (30) alitiwa hatiani kwa makosa 21 ya ubakaji na ujambazi wa kutumia silaha baada ya mfululizo wa matukio yaliyoutikisa mji wa Harare.

Kwa mujibu wa takwimu za polisi, zaidi ta watoto 400 walibakwa na wanawake 392 walinyanyaswa kijinsia mwaka 2013, ambapo wanawake walibakwa wakiwa njiani na watoto wengi walibakwa na majirani au watu wao wa karibu.