FAMILIA NA JAMAA KUKUTANISHWA BAADA YA MIAKA 60

Makundi kadhaa ya watu wakongwe kutoka Korea Kusini wanaelekea Kaskazini kukutana na jamaa zao ambao hawajaonana kwa zaidi ya miaka sitini, tangu vita vilivyotenganisha mataifa hayo mawili ya rasi ya Korea.

Wakongwe hao wamebeba mikoba iliyojaa zawadi, ikiwa ni pamoja na dawa za maradhi ya kawaida, picha za familia na vyakula.

Tukio hilo litakaloibua majonzi litafanyika katika eneo la kitalii upande wa Korea Kaskazini.

Hapajakuwa na zoezi kama hilo lakuunganisha familia tangu mwaka2010.

Awali Korea Kaskazini imefutilia mbali mpango huo wa kuziunganisha familia kujibu vitendo vya Korea Kusini ambavyo Kaskazini inapinga.

Shirika la Msalaba Mwekundu linasema kuwa watu alfu sabini wanaoishi Kusini wanasubiri fursaya kukutana na jamaa zao wa Kaskazini-nusu kati ya watu hao ni wazee walio na umri wa zaidi ya miaka 80.