DAKTARI FEKI AKAMATWA MUHIMBILI

Hospitali ya taifa Muhimbili imemkamata daktari feki hospitalini hapo asubuhi ya tarehe ishirini na tano akiwa na baadhi ya kadi za wagonjwa na vipimo huku historia yake ikionesha aliwahi kuajiriwa na serikali kama utabibu katika hispitali ya amana na Mwananyamala kabla ya kuacha kazi mwaka 1997.

Akitoa taarifa za kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo afisa uhusiano mwandamizi wa hospitali hiyo Bw. Aminieli Aligaesha amemtaja mtuhumiwa huyo kwa jina la Kitano Kitani mwenye umri wa miaka 52 ambaye alijifanya daktari upande wa wazazi alikamatwa bada ya kujaribu kuwatapeli watu mbalimbali hospitalini hapo na amekuwa akionekana mara kwa mara na wagonjwa wengi walidhani kuwa yeye ni daktari halali.

Mtuhumiwa huyo licha ya kukiri kufanya kazi ya utabibu kwa miaka mingi amekana kuhusika na tukio lolote la utapeli hospitalini hapo na kubaini amekuwa akifika hospitalini hapo kwa mambo yake binafsi na kukiri kuendelea kutoa huduma mtaani mara baada ya kuacha kazi ya utabibu.

Raisi wa chama cha madaktari Tanzania daktari Primas Saidia amekiri ongezeko la madaktari feki kwenye hospitali mbalimbali nchini na kushindwa kuthibitisha moja kwa moja kama wanashirikiana na madaktari halali kwenye hospitali husika na kuwa tayri wamejipanga kupambana na matukio hayo kwa kuwapa madaktari mihuri na makoti maalimu yenye nembo ili kuwafanya wagonjwa kutambua nani daktari halali ama la.