MPANDA NAKO WAGOMEA EFD

Wafanyabiashara wa Mji wa Mpanda Mkoa wa Katavi wameungana na wafanyabiashara wenzao hapa Nchini kufunga maduka yao kwa siku mbili kuanzia leo ilikuishinikiza Serikali kusikiliza malalamiko yao ya kiwango kikubwa cha bei za mashine za Kielekroniki za kutoza kodi EFD Wafanyabiashara hao walifikia uamuzi hou baada ya baadhi ya wafanyabiashara wenzao kupita kwenye maduka yao na kuwahimiza kufunga biashara zao za maduka.

Baadhi ya wafanyabiashara hao walisema kwamba wanapinga vikali matumizi ya mashine za EFD kutokana na kwamba ni mzigo kwa wafanyabiashara na zinapatikana kwa gharama kubwa ukilinganisha na mahitaji ya wafanyabiashara wa Mkoa wa Katavi Walisema licha ya machine hizo kuuzwa kwa bei kubwa utengenezwaji wake pia gharama zake ni kubwa kwani pindi zinapoharibika mfanyabiashara analazimika kuwatafuta mafundi kutoka Dares salaam auMbeya ndio waje kutengeneza kwani Mkoa wa Katavi hauna fundi hata mmoja wa kutengeneza mashine hizo.

Mgomo huo ambao ulianza jana umewafanya wananchi wa Mji wa Mpanda wakose huduma mbalimbali walizokuwa wakizihitaji na hasa vifaa vya ujenzi kutokana na maduka yote yanayouza vifaa hivyo yalioko maeneo ya karibu na Soko kuu kufungwa Badhi ya wamiliki wa maduka ambayo hayapo katika orodha ya kutakiwa kutumia mashine hizo kwa kuwa mauzo yao hayafikii shilingi milioni 14 kwa mwaka wamejikuta wakifunga maduka yao kwa kufofia kufanyiwa fujo na wafanyabiashara wenzao.

Kwa upande wake mwenyekitiwa chama cha Wafanyabashara viwanda na kilimo wa Mkoa wa Katavi Hassanali Dalla alisema jana aliombwa na baadhi ya wafanyabiashara wa mji wa Mpanda aitishe mkutano bbaina ya wafanyabiashara na Mkuu wa Mkoa wa Katavi iliwaweze kumweleza msimamo wao wa kupinga mashine hizo.

Alisema hata hivyo aliwapa maelekezo ya kufuata iliaweze kuandaa mkutano huo lakini hadi jana wafanyabiashara hao walikuwa hawajatekeleza utaratibu ambao alikuwa amewalekeza zaidi ya wao kuamua funga maduka yao pasipo kumtalifu mwenyekiti wao.

Pia alisema mpaka sasa mamlaka ya mapato katika Mkoa wa Katavi haijawaandikia barua yoyote wafanyabiashara ambao wanatakiwa watumie mashine hizo hivyo hakuona kama kuna sababu ya msingi ya wafanyabiashara kufunga maduka yao wakati hawana barua yoyote ya kuwaelekeza.