KWA HILI TUMUUNGE MUSEVENI MKONO

TAHARIRI YA MHARIRI WA GAZETI HABARI LEO.

HATIMAYE Rais Yoweri Museveni wa Uganda amesaini Muswada wa Sheria inayopiga marufuku vitendo vya ushoga na kuanzia sasakwa mtu atakayebainika kujihusisha na vitendo hivyo, atakabiliwa na kifungo cha kati ya miaka 14 hadi kifungo cha maisha jela.

Hatua hiyo ya Rais Museveni ni ushindi mkubwa dhidi ya wanaohalalisha vitendo hivyo ambavyo vinaruhusu watu wa jinsia moja kuoana kinyume kabisa na mila na utamaduni wa Mwafrika.

Uganda kwa hilo imethibitisha uhuru wake mbele ya macho ya mataifa ya Magharibi ambayo yamekuwa yakitishia kuibana nchi hiyo kama Rais wake atasaini Muswada huo, yakiongozwa na Marekani.

Hatua ya Serikali ya Uganda imekuja siku chache baada ya Rais wa nchi hiyo pia kusaini Muswada mwingine kuwa sheria ya kupiga marufuku mavazi yanayotia ashiki, ambayo ni vimini na vitopu kwa wasichana.

Hiyo ni dhamira ya dhati kuondoa uhuni na vitendo vinavyokiuka utamaduni wa Mwafrika na hivyo kuifanya nchi kutawaliwa na staha na si ukahaba na umalaya ambao unaichafua jamii ya Kiafrika.

Kuachwa kwa hali kama hiyo iendelee katika jamii, ndiyo sababu sasa tunasikia baadhi ya wasichana wa Afrika Mashariki na hasa Tanzania wanakwenda Mashariki ya Mbali na kujiuza na wengine kuingia katika dawa za kulevya.

Tunampongeza Rais Museveni kwa hatua aliyochukua ya kulinda nchi yake isitumbukie kwenye tabia chafu zinapoigwa kutoka mataifa vya Magharibi ambayo yanadhani haki za binadamu ni pamoja na kukiuka uumbaji alioufanya na kuubariki Mungu.

Wanafanya huku wakijua kabisa kilichotokea Sodoma na Gomora, ambako waliofanya vitendo kama hivyo walilaaniwa; hivyo kuendeleakuunga mkono vitendo hivyo vya kifirauni ni kumuasi Mungu.

Ni vema sasa hata kama Marekani na mataifa washirika wake watapiga kelele, mataifa ya Afrika yakatae vitendo hivyo, ingawa takriban mataifa 14 yanahalalisha kisheria vitendo hivyo kutokana naulevi tu wa kuiga vitendo vya Magharibi.

Hakika kama alivyosema Museveni kama Serikali ya Marekani inapingana na hatua hiyo ya Uganda, basi Taifa hilo kubwa lishirikiane na wataalamu wa Uganda kufanya utafiti na kubaini kama kuna watu walizaliwa wakiwa mashoga.

Akasema kama hilo litathibitika, basi sheria hiyo itapitiwa upya na kubatilishwa, lakini kama hilo halipo basi ni vema kukosa msaadawa Marekani wa dola milioni 400 za Marekani inayopokea kila mwaka badala ya nchi na watu wake kuchafuka.

Tumwunge mkono Museveni kwa ujasiri wake.