MAREKANI NA EU KATIKA MZOZO JUU YA UKRAINE

Tofauti za sera kati ya Marekani na Umoja wa Ulaya kuhusiana na mgogoro wa kisiasa nchini Ukraine zimebainika wazi baada ya kuibuka mazungumzo ya siri baina ya maafisa wawili wakuu wakidiplomasia Kiev.

Mazungumzo yanayotajwa kuwa yalinaswa kisiri kati ya wanadiplomasia wawili wakuu wa Marekani wakizungumzia mstakabali wa Ukraine baada ya tandabelua la kisiasa yameiacha marekani ikionekana Mshari.

Katika mazungumzo hayo yaliyonaswa kisiri naibu waziri wawa mambo ya nje wa Marekani, Sauti ya Victoria Nuland, anasikika akimwambia balozi wa Marekani nchini Ukraine, Geoffrey Pyatt, kuwa hamtaki aliyekuwa mwanamasumbwi, Vitali Klitschko katika serikali ijayo badala yake anasikika akisema 'Yats', akiashiria Arseniy Yatsenyuk ndiye anayepaswa kuwa na usemi mkubwa kutokanana tajriba yake kuu ya kiuchumi na Utawala.

''Yats ndiye anayepaswa Kuingia serikalini na afanye mazungumzona Klitschko mara nne kila juma''

Nuland anasikika akiitusi Umoja wa Ulaya na kusema kuwa Umojawa Mataifa ndiyo unaopaswa kuwa na usemi kuhusiana na hali ilivyo Ukraine kwani Kulinga naye' Umoja wa mataifa ndio unapaswa kusaidia makundi ya upinzani kushikamana

Msemaji katika wizara ya mashauri ya kigeni ya marekani Jen Psaki, hakupinga uhalali wa taarifa hizo.

Msemaji wa ikulu ya White House Jay Carney, amesema kuwa taarifa hizo ziliwekwa kwenye mtandao wa Twitter na afisa wa Urusi.

Kashfa hii ya kidiplomasia inatukia baada mshauri mkuu wa Rais Putin kulaumiwa na Marekani kwa kujiingiza katika siasa Ukraine.

Sergei Glazyev ameilaumu Marekani kwa kutoa mamilioni yadola kwa vyama vya upinzani mbali na kuwakabidhi silaha.

Mshauri huyo wa Putin anasemahatua ya Marekani kuingilia maswala ya ndani ya Ukraine kimsingi inaipa Urusi uhuru na haki ya kuingilia kati.

Rais Putin anatarajiwa kufanya mazungumzo na mwenzake wa Ukraine Viktor Yanukovych wakatiwa michezo ya olympiki ya msimu wa baridi huko in Sochi.