MAKAO MAKUU YA CHADEMA YANUSURIKA KUUNGUA

Makao makuu ya chama cha demokrasia na maendelea Chadema yaliyopo jijini Dar es salaam yamenusurika kuteketea kwa moto baada ya watu wasiojulikana kufanya jaribio la kulipua makao hayo usiku wa kuamkia tarehe 11 Febuari mwaka huu.

ITV imefika katika makao makuu ya chama hicho na kushuhudua askari wa upelelezi wakiendelea na hatua za awali za upelelzi huku katibu mkuu wa chama hicho Dkt Wilbrodi Slaa akilaani kitendo hicho na kutaja tukio Hilo ni mwendelezo wa matukio ambayo yamekuwa yakikikumba chama hicho na kuitaka serikiali kuwa makini na vitendo hivyo kwani vinaweza kuchangia upotevu wa amani hapa nchini.

Aidha Dr Slaa amefafanua kauli yake aliyowahi kuitoa kwa rais Kikwete kuwa kama hata ingilia kati vitendo hivyo nchi haita tawalika kwani itafika kipindi vitendo kama hivyo havitavumilika miongoni mwa Watanzania na kuitaka serikali aingilie kati ili wale wote wanaoendelea kufanya vitendo hivyo wawezea kukamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.


Chanzo:ITV