DK. MTIKILA, PROF. LIPUMBA NDANI YA BUNGE LA KATIBA MPYA

RAIS Jakaya Kikwete ametangaza wajumbe 201 wa Bunge Maalumu la Katiba kwa mujibu wa sheria, huku akiwajumuisha watu mbalimbali wenye umaarufu katika jamii.

Miongoni mwao wamo wanasiasa maarufu wa sasa na wa zamani, wakiwamo wenyeviti wa vyama vyasiasa nchini pamoja na viongozi wa dini, viongozi wa vyama vya wafanyakazi na wanahabari.

Katika wanasiasa wamo, aliyewahi kuwa Waziri tangu enzi za Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, Mzee Kingunge Ngombale-Mwiru, Mwenyekiti wa CUF Taifa, Profesa Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa Tadea, Lifa Chipaka, Peter Mziray (APPT-Maendeleo), Dk Emmanuel Makaidi (NLD), James Mapalala, mwanzilishi wa CUF, Christopher Mtikila (DP), Profesa Abdalla Safari kutoka Chadema, Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro.

Pia wamo wenyeviti wa CCM wa mikoa ya Tabora, Hassan Wakasuvi na wa Iringa, Jesca Msambatavangu, Paul Makonda (Katibu wa Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM), Mwenyekiti wa Wazazi Taifa CCM, Abdallah Bulembo, Mwenyekiti wa CCM Moshi Mjini, Elizabeth Minde, Naibu katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai, aliyekuwa mbunge na Naibu Waziri, Shamim Khan, aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Shaban Muyombo.

Wengine ni ambaye ni Rais wa Chama cha Wakulima Tanzania (AFT), Rashid Yussuf Mchenga, Katibu Mkuu wa Umoja wa Viajana wa CCM(UVCCM), Sixtus Mapunda, wabunge na mawaziri wa zamani Paul Kimiti(Sumbawanga Mjini) na aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Shamsa Mwangunga.

Katika uteuzi huo, Rais Kikwete pia amewateua wanahabari wanne, Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Kajubi Mukajanga, aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Zanzibar, Yussuf Omar Chunda, Mhariri wa Mlimani Media, Hamis Dammbaya na Mwenyekiti wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA), Valerie Msoka.

Aidha, katika uteuzi huo, kundi la viongozi wa dini, Rais amewateua Mussa Kundecha ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, Mjumbe wa Baraza la Ulamaa na Imamu wa Msikiti wa Manyema Dar es Salaam, Hamid Masoud Jongo, Askofu mstaafu wa Kanisa laAnglikana, Donald Mtetemela, Profesa Ricky Costa Mahalu aliyewahi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia.

Katika uteuzi huo, yumo mtoto wa aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, marehemu Dk Sengondo Mvungi, Dk Natujwa Mvungi ambaye amepitia kundi la wasomi akitokea Chuo Kikuu cha Bagamoyo sawa na Profesa Mahalu.

Akitangaza uteuzi huo Ikulu Dar es Salaam jana kwa niaba ya Rais Kikwete aliyefanya uteuzi huo kwa kushirikiana na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein, Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Dk Florens Turuka, alisema Rais amezingatia ushiriki wa watu wa rika zote, na katika hilo, kwa kundi la vijana wa miaka 22 hadi 35, ameteua wajumbe 35; miaka 36 hadi 64 wajumbe 145 na wazee, ameteua 21.

Kwa upande wa uwiano wa kijinsia, Dk Turuka alisema Rais ameteua wanawake 100 na wanaume 101. Aidha, alisema watu 118 walijipendekeza wenyewe majina yao, jambo ambalo ni kinyume chasheria huku majina yaliyopendekezwa na makundi na taasisi mbalimbali yalikuwa 3,636.

Bunge Maalumu la Katiba linatarajiwa kukutana kuanzia Februari 18, mwaka huu mjini Dodoma, likiwa na aina tatu wa wajumbe wa Bunge la Katiba ambao ni wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano; wajumbe wote wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar na wajumbe hao 201 alioteua Rais.

Majina yote kamili haya hapa:


TAASISI ZISIZOKUWA ZA KISERIKALI- (WAJUMBE 20)

TANZANIA BARA (13)

Magdalena Rwebangira ,Kingunge Ngombale Mwiru, Asha D. Mtwangi, Maria Sarungi Tsehai, Paul Kimiti, Valerie N. Msoka, Fortunate Moses Kabeja, Sixtus Raphael Mapunda, Elizabeth Maro Minde, Happiness Samson Sengi, Evod Herman Mmanda, Godfrey Simbeye, Mary Paul Daffa

TANZANIA ZANZIBAR (7)

Idrissa Kitwana Mustafa, Siti Abbas Ali, Abdalla Abass Omar, Salama Aboud Talib, Juma Bakari Alawi, Salma Hamoud Said, Adila Hilali Vuai


TAASISI ZA KIDINI- (WAJUMBE 20)

TANZANIA BARA (13)

Tamrina Manzi, Olive Damian Luwena, Shamim Khan, Mchg. Ernest Kadiva, Sheikh Hamid Masoud Jongo, Askofu Mkuu (Mstaafu) Donald Leo Mtetemela, Magdalena Songora, Hamisi Ally Togwa, Askofu Amos J. Muhagachi, Easter Msambazi, Mussa Yusuf Kundecha, Respa Adam Miguma, Prof. Costa Ricky Mahalu.

TANZANIA ZANZIBAR (7)

Sheikh Thabit Nouman Jongo, Suzana Peter Kunambi, Sheikh Nassoro Mohammed Ibrahimu, Fatma Mohammed Hassan, Louis Majaliwa, Yasmin Yusufali E. H alloo, Thuwein Issa Thuwein.


VYAMA VYOTE VYA SIASA VYENYE USAJILI WA KUDUMU – (WAJUMBE 42)

TANZANIA BARA (28)

Hashim Rungwe Spunda, Thomas Magnus Mgoli, Rashid Hashim Mtuta, Shamsa Mwangunga, Yusuf S. Manyanga, Christopher Mtikila, Bertha Ng'angompata, Suzan Marwa, Dominick Abraham Lyamchai, Mbwana Salum Kibanda,Peter Kuga Mziray, Isaac Manjoba Cheyo, Dr. Emmanuel John Makaidi, Prof. Ibrahim Haruna Lipumba, Modesta Kizito Ponera, Prof. Abdallah Safari, Salumu Seleman Ally, James Kabalo Mapalala, Mary Oswald Mpangala, Mwaka Lameck Mgimwa, Nancy S. Mrikaria, Nakazael Lukio Tenga, Fahmi Nasoro Dovutwa, CostantineBenjamini Akitanda, Mary Moses Daudi, Magdalena Likwina, John Dustan Lifa Chipaka, Rashid Mohamed Ligania Rai.


TANZANIA ZANZIBAR (14)

Ally Omar Juma, Vuai Ali Vuai, Mwanaidi Othman Twahir, Jamila Abeid Saleh, Mwanamrisho Juma Ahmed, Juma Hamis Faki, Tatu Mabrouk Haji, Fat –Hiya Zahran Salum, Hussein Juma, Zeudi MvanoAbdullahi, Juma Ally Khatibu, Haji Ambar Khamis, Khadija Abdallah Ahmed, Rashid Yussuf Mchenga.


TAASISI ZA ELIMU- (WAJUMBE 20)

TANZANIA BARA

Dr. Suzan Kolimba, Prof. Esther Daniel Mwaikambo, Dr. Natujwa Mvungi, Prof. Romuald Haule, Dr. Domitila A.R. Bashemera, Dr. Jasmine Bendantunguka Tiisekwa, Prof. Bernadeta Kilian, Teddy Ladislaus Patrick, Dr. Francis Michael, Prof. Remmy J. Assey, Dr.Tulia Ackson, Dr. Ave Maria Emilius Semakafu, Hamza Mustafa Njozi.

TANZANIA ZANZIBAR (7)

Makame Omar Makame, Fatma Hamid Saleh, Dr. Aley Soud Nassor, Layla Ali Salum, Dkt. Mwinyi Talib Haji, Zeyana Mohamed Haji, Ali Ahmed Uki.


WATU WENYE ULEMAVU- (WAJUMBE 20)

TANZANIA BARA (13)Zuhura Musa Lusonge, Frederick Msigala, Amon Anastaz Mpanju, Bure Zahran, Edith Aron Dosha, Vincent Venance Mzena, Shida Salum Mohamed, Dr. Henry Mwizengwa Nyamubi, Elias Msiba Masamaki, Faustina Jonathan Urassa, Doroth Stephano Malelela,John Josephat Ndumbaro, Ernest Njama Kimaya.

TANZANIA ZANZIBAR (7)

Haidar Hashim Madeweyya, Alli Omar Makame, Adil Mohammed Ali, Mwandawa Khamis Mohammed, Salim Abdalla Salim, Salma Haji Saadat, Mwantatu Mbarak Khamis.


VYAMA VYA WAFANYAKAZI- (WAJUMBE 19)

TANZANIA BARA (13)
Honorata Chitanda, Dr. Angelika Semike, Ezekiah Tom Oluoch, Adelgunda Michael Mgaya, Dotto M. Biteko, Mary Gaspar Makondo, Halfani Shabani Muhogo, Yusufu Omari Singo, Joyce Mwasha, AminaMweta, Mbaraka Hussein Igangula, Aina Shadrack Massawe, Lucas Charles Malunde.

TANZANIA ZANZIBAR (6)

Khamis Mwinyi Mohamed, Jina Hassan Silima, Makame Launi Makame, Asmahany Juma Ali, Mwatoum Khamis Othman, Rihi Haji Ali .


VYAMA VINAVYOWAKILISHA WAFUGAJI-( WAJUMBE 10)

TANZANIA BARA (7)

William Tate Olenasha, Makeresia Pawa, Mabagda Gesura Mwataghu, Doreen Maro, Magret Nyaga, Hamis Mnondwa, Ester Milimba Juma.

TANZANIA ZANZIBAR (3)

Said Abdalla Bakari ,Mashavu Yahya, Zubeir Sufiani Mkanga.


VYAMA VINAVYOWAKILISHA WAVUVI –(WAJUMBE 10)


TANZANIA BARA (7)

Hawa A. Mchafu. Rebecca Masato, Thomas Juma Minyaro, Timtoza Bagambise, Tedy Malulu, Rebecca Bugingo, Omary S. Husseni.

TANZANIA ZANZIBAR (3)

Waziri Rajab, Issa Ameir Suleiman,Mohamed Abdallah Ahmed.


VYAMA VYAWAKULIMA- (WAJUMBE20)


TANZANIA BARA (13)

Agatha Harun Senyagwa, Veronica Sophu, Shaban Suleman Muyombo,Catherine Gabriel Sisuti, Hamisi Hassani Dambaya, Suzy Samson Laizer, Dr. Maselle Zingura Maziku,Abdallah Mashausi, Hadijah MilawoKondo, Rehema Madusa, Reuben R. Matango, Happy Suma, Zainab Bakari Dihenga.


TANZANIA ZANZIBAR (7)

Saleh Moh'd Saleh, Biubwa Yahya Othman, Khamis Mohammed Salum, Khadija Nassor Abdi, FatmaHaji Khamis, Asha Makungu Othman, Asya Filfil Thani.


WATU WENYE MALENGO YANAYOFANANA – (WAJUMBE 20)


TANZANIA BARA (14)

Dr. Christina Mnzava, Paulo Christian Makonda, Jesca Msambatavangu, Julius Mtatiro, Katherin Saruni, Abdallah Majura Bulembo, Hemedi Abdallah Panzi, Dr. Zainab Amir Gama, Hassan Mohamed Wakasuvi, Paulynus Raymond Mtendah, Almasi Athuman Maige, Pamela Simon Massay, Kajubi Diocres Mukajangwa, Kadari Singo.


TANZANIA ZANZIBAR (6)

Yussuf Omar Chunda, Fatma MussaJuma, Prof. Abdul Sheriff ,Amina Abdulkadir Ali, Shaka Hamdu Shaka na Rehema Said Shamte.