WAKANUSHA WABEBA UNGA KUNYONGWA CHINA

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, imekanusha madai kuwa Watanzania 160 wamenyongwa nchini China baada ya kutiwa hatiani kwa makosa ya kusafirisha dawa za kulevya.

"...habari za uhakika kutoka China zinasema Watanzania wenzetu 160 wamenyongwa baada ya kukutwa na hatia ya kusafirisha dawa za kulevya," ilisema taarifa katika mtandao.

Hata hivyo, Mkubwa alisema hadi kufikia Julai mosi mwaka jana, idadi ya Watanzania waliokuwa wanatuhumiwa kwa makosa hayo huko China ilikuwa 176.

Alisema hata kama ingekuwa wamethibitika kutenda makosa na kuhukumiwa kifo, ingekuwa rahisi watu 160 kunyongwa kwa wakati mmoja.

"Inawezekana huyo anayedaiwa kwamba amefariki na ndugu zake wamepata kibali cha kufanya matanga, amekufa kifo cha kawaida akiwa hajahukumiwa, kwa sababu mtu anapohukumiwa kifo na adhabu kutekelezwa, hakuna utaratibu wa ndugu kupatiwa kibali cha matanga," alisema.

Alisema hata hivyo, Serikali kupitia ubalozi wake nchini China, itafuatilia ili kufahamu kinachoendelea dhidi ya watuhumiwa wa kusafirisha dawa za kulevya nchini humo.

Pia alifafanua kuwa Tanzania haina mkataba na China kuhusu kubadilishana wafungwa, na kwamba watakaotiwa hatiani kwa vyovyote watanyongwa hadi kufa kulingana sheria za nchi hiyo.