Wataka Kuruhusiwa Kujiua

Wanaume wawili wenye ulemavu
mbaya zaidi wanakwenda
mahakamani kukata rufaa katika kesi
inayoonekana kuwa moja ya kesi
inayotaka mageuzi makubwa ikitaka
kubadilisha sheria za serikali kuhusu
haki ya mtu kufa.

Mmoja wa watu hao, Pail Lamb
amekuwa na ulemavu mbaya kwa
miaka mingi pamoja na kupitia
uchungu mwingi, hawezi kujitoa uhai
wake na anataka madaktari
waruhusiwe kumuua bila ya
kukabiliwa na kosa la mauaji baadaye.

Mwanamume mwingine anayejulikana
kama Martin, anataka uamuzi
utakaowaruhusu madaktari
wamsaidie kujiua ingawa waweze
kulindwa kutokana na sheria za
kuweza kuwashtaki kwa kufanya
kitendo cha mauaji.

Wakosoaji wanasema kuwa ikiwa
mahakama itaruhusu wawili hao
wajiue, itakuwa na athari kubwa kwa
watu wazee na wenye ulemavu kutaka
kujinyonga ili kuzuia kuwahangaisha
jamaa zao kuwahudumia.