Samatta, Kapombe na Yondani Wagombania Tuzo


WACHEZAJI mahiri wa timu ya
soka ya Taifa ya Tanzania
‘Taifa Stars’, Mbwana Samatta
wa TP Mazembe, Kelvin
Yondani wa Yanga na Shomari
Kapombe wa Simba ya Dar es
Salaam, wametajwa katika
orodha ya wanaowania tuzo ya
Mwanasoka Bora wa Tanzania
mwaka 2012.

Taarifa iliyotolewa kwa
vyombo vya habari jana na
Mwenyekiti wa Kamati ya
Tuzo za Wanamichezo Bora
wa Tanzania mwaka 2012
zinazotolewa na Chama cha
Waandishi wa Habari za
Michezo Tanzania (TASWA),
Haji Manara, ilieleza kuwa
majina hayo ni mapendekezo
kutoka vyama mbalimbali kwa
ajili ya kuwania tuzo hizo kwa
kila mchezo.

Alisema hatua itakayofuata ni
kuchambua majina hayo kwa
ajili ya tuzo hizo ambazo awali
ilikuwa zifanyike Aprili 27
mwaka huu na sasa zitafanyika
mwezi ujao. Orodha kamili ya
wanaowania tuzo kwa mpira
wa magongo wanaume ni
Sylvester Kigodi, Casto
Mayuma, Gurtej Bilu Singh,
Vendri Bhamra na Elias
Samala.

Gofu ya kulipwa wanaume ni
Hassani Kadio, Yassin Salehe,
Fadhili Nkya, Salimu
Mwanyenza na Rajabu Iddy,
wakati gofu ya ridhaa
wanawake ni Madina Idd,
Angel Eaton, Hawa Wanyeche
na Ayne Magombe.

Wanaume ni Jimmy Mollel,
Frank Roman, Nuru Mollel,
Martin MacDonald na John
Said. Ngumi za ridhaa
wanaume ni Ismail Isack
Galiatano, Said Hofu, Selemani
Kidunda, Victor Njaiti,
Mohamed Chibumbui na
wanawake ni Sara Andrew,
Irene Kimaro, Easter Kimbe,
Mather George na Mariam
Nyerere.

Manara aliwataja wanaowania
upande wa ngumi za kulipwa
kuwa ni Francis Miyeyusho,
Ramadhan Shauri, Thomas
Mashali, Said Mbelwa na
Francis Cheka, huku judo kwa
Tanzania Bara wanaume ni
Ahmed Magogo, Andrew
Mlugu, Geophrey Mtawa,
Gervas Chilipweli, Abuu
Mcheteko na Abuubakar Nzige
na wanawake ni Matrida
Temba na Amina Mohamed.

Judo kwa wanaume Zanzibar
ni Mohammed Khamis Juma,
Masoud Amour Kombo na
Mbarouk Suleimani Suleiman,
wakati wanawake ni Grace
Alphonce na Laylati
Mohammed, huku tenisi
wanawake ni Rehema
Athumani, Vailety Peter,
Mkunde Iddi, Edna John na
Zuhura Baraka na wanaume ni
Omary Abdalah, Yassini
Shaabani, Hassan Kassim,
Kiango Kipingu na Lebric
Jacobu.

Mpira wa mikono kwa
wanaume na timu zao katika
mabano ni Faraji Shaibu
(Nyuki Zanzibar) Hemedi
Salehe na Abinery Kusena
(JKT), Ally Khamis (Ngome) na
Hassan Yusufu (Magereza),
wakati wanawake ni Catherine
Mapua (Ngome), Doris
Mangara (Magereza), Zakia
Mohammed (Ngome), Happy
Mahinya (JKT) na Mary Kimiti
(Magereza).

Riadha wanawake ni Zakia
Mrisho, Mary Naali, Jackline
Sakilu, Sarah Ramadhani,
Anjelin Tsere, Sara Maja,
wanaume ni Dickson Marwa,
Faustine Musa, Augustino Sule,
Bazil John na Samson
Ramadhan.

Kriketi wanaume
ni Abhik Patwa, Benson Mwita,
Sefu Khalifa, Issa Kikasi na
Riziki Kiseto, wakati
wanawake ni Monica Pascal,
Mwanaiddi Ibrahim, Hadija
Nasibu, Esther Wales na
Mwanaidi Ammy.

Soka wanawake ni Fatuma
Mustapha, Asha Rashid,
Mwanahamisi Omary, Sophia
Mwasikili na Ester Chabruma,
wanaume ni John Bocco
(Azam), Kelvin Yondani
(Yanga), Shomari Kapombe
(Simba), Mcha Khamisi
(Azam), Mbwana Samatta (TP
Mazembe).

Wachezaji wa nje wanaocheza
Tanzania ni Emmanuel Okwi-
Simba (sasa Etoile du Sahel),
Kipre Tchetche-Azam, Haruna
Niyonzima na Hamisi Kiiza,
wote Yanga na Mary Waya
(netiboli-alikuwa kocha
mchezaji).

Upande wa kikapu ni Faraja
Malaki (Jeshi Stars), Evodia
Kazinja (JKT Stars), Doritha
Mbunda (JKT) na Sajida Ahmed
(Don Bosco) wakati wanaume
ni Mussa Chacha, Lusajo
Mwaipopo na Erick Mchemba.

Netiboli ni Lilian Sylidion
(Filbert Bayi), Mwanaidi
Hassan (JKT), Irene Kanile
(Filbert Bayi), Jacqueline
Sikozi (Filbert Bayi), Faraja
Malaki (Jeshi Stars).

Wachezaji Bora Chipukizi ni
Salum Abubakari (Azam),
Frank Domayo (Yanga),
Edward Cristopher (Simba) na
Emmanuel Malya tenisi Arusha,
wakati Watanzania
wanaocheza nje ni Mbwana
Samatta (TP Mazembe), Ivo
Mapunda (Gor Mahia),
Hasheem Thabeet (Oklahoma),
Thomas Ulimwengu (TP
Mazembe), Soud Abdulrazak
na Mohammed Abdallah
‘dulah’ (wote Uganda).

Chanzo:Habari Leo