Akamatwa na Vifaa Vya Kutengenezea Hela Bandia

Jeshi la polisi mkoa wa  Katavi
limemkamata Hilali  Abdalah
(30) mkazi wa mtaa wa majengo
mjini hapa kwa kumkamata
akiwa na vifaa vya kutengenezea
noti  bandia   akiwa katika nyumba
ya kulala wageni
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa
Katavi Dhahiri Kidavashari alisema
Hilali alikamatwa hapo jana majira
ya  ssa 8 mchana katika nyumba ya
kulala wageni inaitwa
Ambassodor aliyoko  katika mtaa
wa mji wa  zamani  Kata ya
kashaulili  mjini hapa
Alisema mtuhumiwa alikamatwa
kufuatia taarifa za kiitelejensia
kulifikia jeshi la polisi mkoa wa
Katavi kutoka kwa raia wema
kuwa Hilali anajihusisha na
shughuli hiyo ya utengenezaji wa
noti bandia.

Kidavashari alivitaja vifaa
aliwavyo kamatwa navyo
mtuhumiwa kuwa ni  karatasi
ngumu  217 ambazo hutumika
kutengenezea   noto bandia za
shilingi  10,000  bomba mbili  za
sindano zenye dawa maalumu
kwa ajiri ya kubadilishia  rangi ya
karatasi hizo ili zifanane na pesa
hizo.

Alivitaja vifaa vingine kuwa ni
powder chupa moja  kwa ajili ya
ya kumfanya mteja ataakizishika
mapema zisiache alama ya
vidole kwenye pesa beseni  moja
jeusi kwa ajiri ya kusafishia
karatasi hizo mara baada ya
kuzipitishia  kwenye hatua kadha
vifaa ningine alivyo kamatwa
navyo Hilali ni karatasi 21 plain
kwa ajiri ya kufunikia karatasi
ngumu zisipate hewa wakati wa
utengenezwaji wa noti   bandia
soltap 2  kwa ajiri ya kubania
karatasi zisipate hewa mapema
pasi moja ya umeme  kwa ajili ya
kukaushia pesa  hizo  mara baada
ya kuziosha na ugolo vijiko
vitatu   ambao alikuwa akiutumia
kama kilevi wakati akifanya
shughuli hiyo  haramu.

Kamanda waa polisi mkoa wa
Katavi alieleza  awali  mtuhumiwa
alikuwa akijishughulisha na
shughuli za  kuuza mitumba
kaika soko la Buzogwe mjini hapa
na baadae alihamia mkoani
Tanga  na ndiko aliko patia ujuzi
wa kutengeneza noti bandia
Kidashari alieleza  hatimaye baada
ya kupata utaalamu huo alirejea
Mpanda na kuanza  kazi  hiyo
mbaya ya kuvunja sheria za
Nchi.

Alisema katika  maelezo yake ya
awalialikiri kufanya shughuli hiyo
kwa kile alicho kieleza ni
kutokana na yeye  hapo siku za
nyuma aliwahi kutapeliwa pesa
kwa kupewa noto bandia ndio
maana ameamua na yeye kulipa
kisasi kwa watu wengine
Pia mtuhumiwa alitaja sababu
nyingine kuwa ni katika kujitafutia
maisha  kwa njia ya ytafuataji ndio
maana akaamua kujitafutia pesa
kwa njia hii
mtuhumiwa anategemewa
kufikishwa mahakamani  mara
upelelezi wa kesi hii utakapo
kamilika ili aweze kujibu
mashitaka yanayo mkabili.

Chanzo:kataviyetu.blogspot.com