Mapambano ya Mtwara

MTWARA : GESI GESI WAR UPDATE
*. Kuna madai ambayo hayajathibitishwa kwamba wanawake wanabakwa na
maaskari, wanapigwa risasi kutokana na vijana wote kukimbia maporini.
*. Mwanamke anayekadiriwa miaka 25 mjamzito auawa kwa kupigwa risasi
maitiipo Ligula.

*. Mwanafunzi wa CHUNO afikishwa hospitali Ligula na majeraha ya risasi mguuni.
*. Maduka maeneo ya Magomeni yamechomwa moto ikiwamo pia mali za
Askari magereza na uhalifu ukifanyika vidole vinawaelekea Polisi.

*. Afisa Usalama wa Taifa ambaye anamiliki nyumba ya wageni naye
amevamiwa na kuporwa mali ikiwamo fedha katika gesti yake.
Haijajulikana ni kiasi gani cha mali kilichopotea.
*. Mabomu yanaendelea kupigwa tofauti kwa sasa hayapigw mfululizo.

*. Mabomu yametulia. Hali ya ukimya imetawala.
*. Mabasi 5 ya Champion yamebeba Wanajeshi yako njiani yanakuja.
*. Serikali yatoa tamko yasema watu 91 wanashikiliwa.

*. Bunge laahirishwa tena. Kupisha uchunguzi na kuepusha uchochezi
kutoka kwa baadhi ya wabunge. (Kwa mujibu wa Spika)
*. Maeneo ya Magomeni, Chikongola, Nkanaledi, Mikindani maaskari
wanaingiamajumbani mwa watu na kumsomba mtuyeyote ambaye ni mwanaume
awe amehusika awe hajahusika na kumkamata. Pia inaripotiwa na uhalifu
unafanywa na maaskari hao hao. Jambo linaloamsha hisia kwa wananchi.

*. RPC anaongea na vyombo vya habari na kuwasihi wananchi waende
makazini. Lakini kiuhalisia hali sio shwari.
*. Mahakama ya mwanzo ya Mitengo imechomwa moto

*. Mpaka sasa ni vita baina ya wananchi na maaskari. Mabomu yamesikika
pamoja namilio ya risasi masaa 24. Na milio ya Risasi na mabomu
inaendelea kusikika.

*. Raia wapatao 7 wameripotiwa kufariki (wengine walipelekwa hospitali
ya Ndanda Ndogo na mmoja ameripotiwa kupokelewa Ligula.

*. Nyumba za viongozi zinaendelea kuchomwa moto.
*. Majibizano baina ya Polisi na Raia yanaendelea maeneo ya Magomeni,
Nkanaledi na Mikindani.

*. Maduka yamefungwa na hakuna huduma zozote
Barabara zimewekwa vizuizi magogo na matairi yamechomwa moto. Hakuna
njia yakupita.



chanzo:mtwarakumekucha.blogspot.com