Vurugu za Mtwara

Mtu moja anamefariki dunia katika vurugu zinazoendelea mjini mtwara.

Na wakati huo huo nyumba nne (4) zaripotiwa kuchomwa na waandamanaji nyumba moja ikiwa ni ya Mbunge na moja ya mwandishi wa habari wa Tbc, pia nyumba nyingine yadaiwa kuwa ni ofisi ya CCM iliyopo karibu na Chuo cha Uhasibu(TIA) Sambamba na uchomaji huo pia kituo cha kuuzia mafuta cha total nacho pia Charipotiwa kuwa kimechomwa moto.

Polisi wamelazimika kutumia mabomu ya machozi na risasi za moto ilikuweza kuwatawanya waandamanaji hao.

Vurugu zimekuja baada ya kusomwa kwa bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini leo mjini dodoma. Ambapo imekuwa kinyume na matarajio mengi ya wanamtwara.

Vurugu hizo zimesababisha kwa kufungwa kwa barabara ya Dar-Mtwara na kuvunjwa kwa daraja linalo unganisha Mtwara na Lindi ambapo magari huishikia katika mkoa wa Lindi.

Raia wa kigeni kadhaa
waliokuwa wakiendelea na
shughuli mbalimbali katika
bandari ya mtwara
wameonekana wakiondoka