The Bavarians Mabingwa Wapya Ulaya

Hatimae timu kutoka Jijini Münch The Bàvarian Bayern Münich wamefanikiwa kuchukua ubigwa wa ligi ya mabigwa ulaya kwa mara ya tano(5)

Bayern imepata ubingwa baada ya kuwapa kichapo ndugu zao Borussia Dortmund kwa goli mbili kwa moja.

Bayern walikuwa wa kwanza kupata goli kupitia kwa mcroatia Mario Mandzükic katika dakika ya 60 akipokea mpira kutoka kwa Arjen Robben.

Dakika nane baada Dante Borim alimchezea vibaya Marco Reuc na kusababisha penati ambapo Gündogan aliweka wavuni na kufanya matokeo kusomeka 1-1 katika dakika ya 68.

Alikuwa ni Arjen Robben ambaye alipeleka shangwe kwa Munchen katika dakika ya 89 ya mchezo kwa kupachika goli maridadi baada ya juhudi binafsi kutumika.

Bayern wanaungana na Madrid, Ac Milani na Liverpool kuchukua Ubigwa wa ulaya zaidi ya mara tano. Madrid anaongoza kwa kuchukua mara 9 akifuatiwa na Ac Milan ambao wamenyakua mara saba(7) huku Bayern na Liverpool wakiwa wamechukua mara tano kila mmoja.

Barcelona wanafuata kwa kuchukua mara nne(4) Manchester united mara tatu(3) na timu nyingine kutoka uingereza ya N.Forest wakichukua mara mbili(2) na Chelsea mara moja.
Hongera kwa Bayern Münich.