Shekh Amwagiwa tindikali huko Zanzibar.

Sheha wa Tumondo
Mohamed Omary
Said, amemwagiwa tindikali na mtu
asiyejulikana na hivyo kupata
maumivu makali sehemu yake ya
kifua na jicho kuumia pia.
Sheha huyo alikimbizwa katika
Hospitali ya Mnazi mmoja mjini
Unguja ambapo alipatiwa matibabu
ya dharura.

Kamanda wa polisi wa Mkoa wa
Mjini Magharibi,Mukhadam
Khamis,amesema chombo
kilichotumika kumwagia tindikali
Sheha huyo kilipatikana eneo la
tukio na kwamba polisi imekichukua
kwa kukichunguza kitaalam ili
kugundua aliyekuwa akikitumia kwa
kuangalia alama za vidole.

Sheha huyo alimwagiwa tindikali
jana usiku wakati alipotoka nje ya
nyumba yake kuchota maji na ndipo
mhalifu huyo alipomwagia tindikali
na kwamba hakuweza kumtambua.