Babu Wa Loliondo anaswa Bank

Katika kuonesha kuwa Mchungaji
Mstaafu, Ambilikile Mwasapile ‘Babu
wa Loliondo’ bado ana fedha baada
ya kuzikusanya kutoka kwa wateja
wake wa huduma ya kikombe, hivi
karibuni alinaswa ndani ya Benki ya
NMB akipata huduma.

Babu alibambwa ndani ya benki
hiyo Tawi la Loliondo mkoani
Manyara akihudumiwa na mmoja
wa wafanyakazi aliyefahamika kwa
jina la Lembris Lesion ambapo
inaelezwa alikuwa akielekezwa jinsi
ya kujiunga na huduma mpya ya
Jisevie.

Akiwa benki hapo, Babu alionekana
akijaza fomu huku akiwa na begi
ambalo linashukiwa kuwa na fedha
ndani yake ambapo baadhi ya watu
waliokuwa wakimpiga chabo
hawakuonesha kumshangaa
wakiamini bado ana mkwanja wa
kutosha kutokana na ile tiba
ailiyokuwa akiitoa kwa watu wengi
hivi karibuni.

“Unajua Babu alipata pesa nyingi
sana na bado anaendelea
kuzikusanya, kimsingi ana pesa
ndefu benki,” alisema mmoja wa
wateja aliyekuwa eneo hilo.

Source: udakuspecial