Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Chiganga Ntengwa baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka, ukiongozwa na Mwendesha Mashtaka, Godfrey Luzabila.Hakimu alisema ushahidi uliotolewa mahakamani na upandewa mashitaka pamoja na mashahidi watatu, ikiwemo taarifa ya uchunguzi wa kitabibu, zimethibitisha mama huyo alikuwa amebakwa na kuharibiwa sehemu za siri.
"Hivyo Mahakama haikuona shaka lolote kukutia wewe mshtakiwa hatiani " alisema hakimu.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Agosti 18 mwaka jana saa 12 jioni kijijini Ifukutwa Tarafa ya Kabungu wilayani Mpanda.
Ilidaiwa kuwa mtu huyo, ambaye wakati huo alikuwa kibarua wa kuchimba mitaro ya barabara, alimwona mama huyo akipita barabarani, karibu na alipokuwa akifanya kazi.
Alimvamia kisha akamvuta kichakani na kumbaka. Kwa mujibuwa Hakimu Ntengwa, licha ya mama huyo kumsihi mshitakiwa akatafute mwanamke mwingine warika lake, alikaidi na kuendelea kumshika kwa nguvu kisha kumvua nguo zake za ndani. Mama huyo alipiga yowe kuomba msaada.
Ilielezwa kuwa yowe hizo zilisababisha wapita njia watatu kumsikia.
Waliamua kufutilia kichakani na kukuta akifanya kitendo hicho, wakamkamata.
Chanzo: Habari leo