AJARI YAUA KIONGOZI WA KANISA KUELEKEA SHEREHE ZA KUSIMIKWA MKUU WA JIMBO MPANDA

Kwa habari zilizotufikia hivi punde ni kuwa father Kapufi na Katekista mmoja(jina halijafahamika) wamefariki dunia kutokana na ajari ya gari waliyopata wakitokea Inyonga kuja mpanda mjini kuhuzuria kusimikwa kwa mkuu wa jimbo katoliki la Mpanda askofu G. Nyaisonga.

Askofu Gervas Nyaisonga (48)anasimikwa kesho siku ya jumapili kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Mpanda katika ibada inayotarajiwa kufanyika kuanzia saa nne asubuhi katika viwanja vya shule ya chekechea inayomilikiwa na Kanisa Katoliki jimbo la Mpanda.


Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na uongozi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mpanda ibada ya kusimikwa Askofu Nyaisonga itahudhuriwa na Maaskofu wote wa Kanis hilo na mapadri watawa na walei wa kutoka majimbo mbalimbali ya kanisa hilo.


Askofu Nyaisonga anahamia jimbo Katoliki la Mpanda kabla ya hapo alikuwa ni Askofu wa Jimbo la Dodoma jimbo la Mpanda lilikuwa halina Askofu toka mwaka juzi kufuatia kufariki kwa aliyekuwa Askofu wa jimbo hilo Paskal Kikoti kufariki Dunia hapo mwaka juzi

Jimbo Katoliki la Mpanda lilianzishwa mwaka 2001 na Askofu wake wa kwanza wa Jimbo hilo alikuwa ni marehemu Paskali Kikoti hinyo Askofu Gervas Nyaisonga atakuwa ni Askofu wa PILI tangia jimbo katoliki laMpanda lilipoanzishwa.


Katika ibada hiyo ya kusimikwa kwa Askofu Nyaisonga Serikari itawakilishwa na Waziri wa Nchi ofisi ya waziri Mkuu uwekezaji na uwezeshaji MeryNangu ambae atatowa salamu za Serikali kwenye ibada hiyo.


Miongoni wa watakao hudhuria ibada hiyo hapo kesho ni Mke wa Waziri Mkuu Mama Tunu Pinda na viongozi mbalimbali wa Serikali wa Mkoa wa Katavi na Viongozi wa mikoa ya jirani ya Rukwa Tabora na Kigoma.