WACHEZAJI WATANO WA KIGENI RUKSA

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara imeamua msimu ujao klabu zinazoshiriki ligi hiyo kusajili wachezaji watano wa kigeni badala ya wachezaji watatu.

Awali, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) lilitaka kupunguza usajili wa wachezaji wa kimataifa kutoka watano hadi watatu ili kutoa nafasi kwa wachezaji wazawa kucheza zaidi.


Mabingwa wapya Azam tayari ina wachezaji watano ambao ni Brian Umony (Uganda), mapacha Kipre Tchetche na Kipre Balou (wote kutoka Ivory Coast) na hivi karibuniimesajili mshambuliaji kutoka Mali,Ismailla Diarra kwa mkataba wa miaka miwili na Didier Kavumbagu (Burundi) akichukua nafasi ya Mohamed Kone waliye mfungashia virago.

Taarifa za kubakisha wachezaji watano zitakuwa shangwe kwa Yanga, ambao walidai kupokwa Kavumbagu kwa vile sheria mpya ya TFF ya kutaka kubaki wachezaji watatu ndio iliyowabana na kusababisha kushindwa kuwapa mkataba kwa wakati Kavumbagu na Mbuyu Twite, ambaye usajili wake unasubiri maamuzi hayo.

Akizungumza kuwapo kwa taarifa za kubaki kwa kipengele hicho, mmoja kati ya viongozi wa TFF, ambaye hakutaka jina lake kuandikwa kwa kutokuwa msemaji, alisema Bodi ya Ligi imependekeza kuwa na wachezaji watano kwa misimu mitatu mfululizo.


"Azam wanashiriki Ligi ya Mabingwa mwakani, halafu Azam ni wadhamini wa Ligi Kuu Bara, kuna mambo mengi yameangaliwa ikiwamo ligi yetu kuwa bado changana wachezaji wa kigeni ndio wamekuwa wakitoa changamoto na kuleta ushindani kwa wachezaji wetu wa ndani na kuifanya ligi iwe angalau na mvuto," alisema.


Hata hivyo, licha Bodi ya Ligi kupitisha mapendekezo hayo, TFF ambao ndiyo wasimamizi wa mpira nchini watakutana na klabu za Ligi Kuu Mei 11 na kuwaeleza maazimioya Kamati ya Utendaji ya TFF ambayo ilikaa jana, pia watajadili mikataba mbalimbali ya ligi na kuangalia namna ya kuiboresha.

Pendekezo la kutumia wachezaji watatu katika ligi msimu ujao lilikuwa ni utekelezaji wa Azimio la a Bagamoyo ambalo limeonekana kuwa gumu kutekelezeka.


Mwaka 2007 TFF kwa ufadhili wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa)iliandaa semina mjini Bagamoyo ikishirikisha viongozi wa klabu na wadau wa soka na kufikia makubaliano ya timu za Ligi Kuu kuwa na idadi ya wachezaji wa kigeni wasiozidi watatu ili kuwapa nafasi wazawa.

Pendekezo la timu za Ligi Kuu kuwa na wachezaji wa kigeni wasiozidi watatu lilipaswa kuanza kufanyiwa kazi msimu wa Ligi Kuu yaTanzania Bara uliomalizika hivi karibuni, lakini ilishindikana baada ya baadhi ya timu kuomba kuongezwa muda wa msimu mmoja kabla ya utekelezaji wake na hivyo lilitakiwa lianze kutumika msimu ujao, ambapo pia limegonga mwamba.


Akizungumzia suala hilo la usajili wa wachezaji watano wa kigeni, msemaji wa Yanga, Baraka Kizuguto

alisema: "Bado hatujapata mwongozo wowote kutoka TFF lichaya kuomba, hata hivyo Mei 11 kunakikao cha klabu za Ligi mambo yoteyataamuliwa huko."


Kwa upande wake, Meneja wa Azam FC, Jemedari Said, alisema: "Suala hilo ni kubwa kwangu, viongozi wa juu ndio wanahusika nalo zaidi, Jumatatu tuna kikao kule(TFF), ndio kila kitu kitajulikana."

Katibu wa Simba, Ezekiel Kamwaga hakuweza kupatikana kuzungumzia suala hilo.