AJARI YA FUSO YAUA WATATU NA KUJERUHI

Watu watatu wamefariki dunia hapo hapo Wilaya Mpanda Mkoa wa Katavi baada ya gariRoli aina ya Fuso walilokuwa wakisafiria kupinduka na watu wengine wanne wamejeruhiwa na kulazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda.

Ajari hiyo ilitokea hapo juzi majira ya saa kumi na moja jioni baada ya gari aina ya fuso lenye Nanba za usajiri T 168 APU lililokuwa likiendeshwa na Dreva Deus Lukas (28 )mkazi wa mtaa waKawajense Mjini hapa kupinduka katika mlima wa Sijonga Gari mali ya mtu mmoja mkazi wa kijiji cha Ikola alifahamika kwa jina moja tuu (MAN) Katika ajari hiyo watu watatu walikufa hapo hapo ambao Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwataja kuwai ni Agnes Martin(7) mwanafunzi wa shule ya Msingi Kashato katika Halmashauri ya mji wa Mpanda Elizabeti Mseveni (24) mkazi wa Mtaa wa Majengo mjini Mpanda ambae ni mama mdogo wa Agnes na Madanganya Rashid (53) mkazi wa kijiji chaIkola Tarafa ya Karema Wlaya ya Mpanda Kamanda wa Jeshi la Polisi waMkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari alisema ajari hiyo ilitokea katika eneo la Mlima wa Sijonga Katika Tarafa ya Kabungu Barabara inayotoka mjini Mpanda Kuelekea Tarafa ya Karema mwambao mwa Ziwa Tanganyika baada ya gari hilo kukatika propela shafuti likiwalikiwa kwenye mlima Kidavashari aliwataja watu wanne waliojeruhiwa ambao wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda kuwa niSaimoni Masafila (42)Mkazi wa Kijiji cha Mwamapuli Tarafa ya Mpimbwe Wilaya yaMlele Mwasiti Juma (19) Mwajuma Seif (19) na Nassir Salumu mtoto mdogo wa miezi minne wote wakazi wa mjini Mpanda


Alisema Dereva wa gari hilo Deus Lukas alikuwa akiendesha Fuso hilo huku akiwa amewapakia watu hao na mizigo mbalimbali ya bidhaa za wafanyabiashara huku akiwa anatokea mjini Mpanda akiwa anaelekea katika kijiji cha Ikola kilichoko mwambao mwa ziwa Tanganyika


Kidavashari alifafanua baadaya gari hilo kufika kwenye eneo la mlima wa Sijonga gari hilo lilikatika propela shafti na kusababisha roli hilo kupinduka na watu watatu walifariki Dunia hapo hapo na watu wanne walijeruhiwa nakulazwa katika hospitali ya Wilaya ya Mpanda wakiendelea kupatiwa matibabu huku hari zao zikiwa zinaendelea vizuri.

Alisema Dereva wa Gari hilo alikamatwa na anaendelea kushikiliwa na jeshi la polisi wakati taratibu za kumfikisha mahakamani zikiwa zinaendelea ili akajibu mashitaka ya kuhusiana na ajari hiyo.

Kidavashari alieleza mili ya marehemu wote watatu imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda kwa ajiri ya kufanyiwa uchunguzi wa Kidaktari na baada ya hapo watakabidhiwa ndugu kwa ajiri ya mazishi.