WATU 46 WAUAWA KATIKA MILIPUKO KATIKA MJI WA JOS

Takriban watu 46 wameaga dunia na wengine wengi kujeruhiwa baada ya milipuko miwili mikubwa kutokea nchini Nigeria katika mji wa Jos.Milipuko hiyo imetokea katika soko lenye shughuli nyingi .
Mwandishi wa BBC aliyeko huko anasema kuwa amehesabu miili 40 ikipelekwakatika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali moja iliyoko JOS.




Mwandishi wa BBC Ishaq Khalid aliye mjini humo anasema kuwa kuna hofu ya watu wengi kujeruhiwa hasa kwa kuwa soko hilo lilikuwa na idadi kubwa ya watu.

Aidha anaarifu kuwa taharuki ietanda katika eneo hilo baada ya vijana waliopandwa na hasira kufunga mabarabara ya kuingia na kutoka mjini humo na kuzua hofu ya makabiliano.
Mji wa Jos itakumbukwa iliwahi kushuhudia mapigano mabaya zaidi baina ya makundi ya vijana Waislamu na wale Wakristu iliyosababisha maafa mengi.
Mabomu hayo yanasemekana kuwa yalikuwa yametegwa moja katika lori na lingine katika gari la uchukuzi wa abiria na yakalipuka kwa mpigo moja katika soko la lingine karibu na hospitali.
Hakuna aliyekiri kutekeleza mashambulizi hayo ijapokuwa jimbo hilo limewahi kushambuliwa na kundi la Boko Haram zaidi ya miaka miwili iliyopita.


Jimbo la Platue liko mpakani kati ya waislamu wanaoishi Kaskazini mwa Nigeria na Wakrstu ambao wanaishi Kusini .
Jimbo hili limewahi kushudia mapigano baina ya wakulima wakristu wa tabaka la Berom na waislamu wafugaji wa kuhamhama wa tabaka la Fulani.
Mnamo mwezi Machi mwaka uliopita kituo cha basi kilishambuliwa kwa bomu na awali mwaka wa 2012, Boko Haram walifanya shambulio baya zaidi lililowaua zaidi ya watu 150 katika msururu wa milipuko.
Kundi hilo bado linawazuilia wasichana zaidi ya 200 wa shule, lililowateka kutoka kijiji kimoja kaskazini mashariki mwa Nigeria mwezi mmoja uliopita.
Nchi kadhaa zikiwemo Uingereza, Ufaransa na Marekani wameahidi kutuma wanajeshi kusaidia kuwakomboa wasichana hao.
Nao viongozi wa Afrika wanaokutana mjini Paris wametangaza 'vita' dhidi ya Boko Haram na kuahidi kushirikiana ki-intelijensia na kijeshi, kupambana na Boko Haram.