GAVANA WA NAIROBI ATIMULIWA

Gavana wa mji mkuu wa Kenya Nairobi, Evans Kidero ametimuliwa mamlakani na mahakama ya rufaa.

Mahakama hiyo, imeamua kuwa Kidero na naibu wake Jonathan Mueke hawakuchaguliwa kihalali.


Uamuzi huo ulitolewa kufuatia ombi la waziri msaidizi wa zamani Ferdinand Waituti ambaye aliwania kiti hicho wakati wa uchaguzi mkuu mwaka 2012.


Gavana Kidero alisifika wakati mmoja kwa tukio la kumzaba kofi mwakilishi wa wanawake nchini Kenya Rachel Shebesh walipodai kuwa alivamia ofisi yake akiwa ameambatana na na wafanyakazi wa baraza la jiji waliokuwa wanadai kushughulikiwa kwa maslahi yao ya kikazi.