AFARIKI BAADA YA KUZIDISHA KUNYWA VIROBA

Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Michael Silanda (26 ) Mkazi wa Kijiji cha Ibindi Tarafa ya Nsimbo Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi amefariki Dunia baadaya kunywa Pombe (VIROBA ) aina ya Zed kupita kiasi bila kula Kwa mujibu wa Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa Kamishina msaidizi mwandamizi Dhahiri Kidavashari tukio hilo lilitokea hapo mei tano mwaka huu majira ya saa sita usiku kijijini hapo.


Alisema siiku hiyo ya tukio marehemu baada ya kuamka asubuhi nyumbani kwake hapo majira ya saa tano asubuhi alielekea kwenye Bar ambayo ilikuwa ikiuza vinywaji vya aina mbalimbali vya pombe kali na vinywaji baridi.


Alifafanua kuwa baada ya kufika kwenye Bar hiyo aliwakuta baadhi ya wanakijiji wenzake wakiwa wanakunywa pombe za aina mbalimbali hari ambayo ilimfanya marehemu aweze kujumuika nao kwa kuagiza pombe (VIROBA ) aina ya Zed.


Alisema Michael aliendelea kunywa viroba kuanzia mudahuo kwenye bar hiyo bila kula kitu chochote hadi hapo majira ya saa sita usiku alipoamua kurudi nyumbani kwake huku akiwa amelewa pombe kupita kiasi.


Baada ya kufika nyumbani kwake aliingia ndani ya nyumba yake na kulala bila kula chakula chochote na siku iliyofuata majira ya saa mbili asubuhi ndipo walipomkuta Michael akiwa amefariki Dunia huku akiwa amelala kitandani kwake.


Kamanda Kidavashari alisema uchunguzi wa awali oliofanywa kuhusiana na kifo hicho umebaini kuwa kifo hicho kimesababishwa na marehemu kunywa pombe nyingi kupita kiasi bila kula chakula.


Alisema mwili wa marehemu Michae Silanda umehifadhiwa kwenye chumba cha kuifadhi maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda kwa ajiri yakufanyiwa uchunguzi wa Kidaktari na baada ya uchunguzi huo watakabidhiwa ndugu wa marehemu kwa ajiri ya utaratibu wa mazishi.