AHUKUMIWA JELA MIAKA 30 KWA UBAKAJI

Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi imemuhukumu Philipo Emanuel (35) Mkazi wa Mtaa wa Mpanda Hotel mjini Mpanda kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na kosa la kumbaka shemeji yake msichana (13) mdogo wa mke wake mdogo.

Hukumu hiyo imetolewa hapo juzi na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama ya Wilaya ya Mpanda Chiganga Ntengwa baada ya mahakama kulidhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na pambe zote mbili za upande wa mashitaka na utetezi

Mshitakiwa alidaiwa kutenda kosa hilo la kumbaka mdgo wa mke wake hapo Septemba 24 mwaka jana majira ya saa moja na nusu usiku huko katika eneo la mtaa wa Nsemulwa mjini Mpanda.

Awali katika kesi hiyo mwendesha mashitaka Godfrey Ruzabila aliiambia mahakama kuwa siku hiyo ya tukio msichana huyo aliyebakwa alikuwa ametumwa dukani na dada yake kwenda kununua mafuta ya kupikia mlo wa jioni.

Alieleza wakati msichana huyo akiwa anaelekea dukani ndipo alikutana na mshitakiwa ambae alimwita msichana huyo na kisha alimwomba amsindikize dukani alikokuwa anakwenda kununua mafuta ya kula aliyokuwa ametumwa na dada yake.

Mwendesha mashitaka alidai baada ya kuwa wamefika dukani msichana huyo alinunua mafuta na kisha mshitakiwa alimweleza shemeji yake kuwa anataka kumnunulia zawadi dukani hapo hivyo achague kitu gani anachokihitaji ndipo msichana huyo alipomweleza shemeji yake kuwa yeye anahitaji Biscut na Pipi bomu

Mshitakiwa baada ya kumnunulia shemeji yake zawadi hizo alimtaka amsindikize alikokuwa akienda ombi ambalo msichana huyo alilikubali kwani hakuwa na mashaka yoyote ya kusindikizwa na shemeji yake.

Mwendesha mashitaka alieleza wakati wakiwa njiani mshitakiwa Philipo Emanuel alimwingiza msichana huyo kwenye pagara na kisha alipiga ngwala na kuanza kumbaka huku msichana akijaribu kupiga mayowe ya kuomba msaada lakini alishindwa kutokana na mshitakiwa muda wote kuwa amembana mdomo.

Alieleza baada ya kuwa amemaliza kumfanyia unyama huo alipatia mtoto huyo shilingi elfu moja kama malipo yake na shilingi elfu tano alimpatia ili amfikishie dada yake na alimkaza asimwambie mtu yoyote yule kuwa amefanyiwa kitendo hicho na mshitakiwa.

Ruzabila alisema baada ya msichana kufika nyumbani kwao dada yake alimuuliza kwanini amechelewa kurudi ndipo binti huyo alimweleza dada yake njisi ambavyo shemeji yake alivyomfanyia hari ambayo ilmshitua dada yake na kumfanya achukue uamuzi wa kumvua nguo na kumkagua katika sehemu zake za siri na kukuta anatokwa na damu hari ambayo ilimfanya ashituke na kupelekea kuamua kutoa taarifa kwa wapangaji wenzake.

Alieleza dada wa binti na majirani walimtaka msichana huyo awapeleke kwenye eneo alilofanyiwa unyama huo na walipofika kwenye eneo la tukio waliingia ndani ya pagala na kukuta Paketi ya Biscuti aliyokuwa amenunuliwa na shemeji yake huku pembeni kukiwa na mafuta ya kula yaliyomwagika na ndipo walipo amua kwenda kituo cha polisi cha mpanda na kutoa taarifa.

Katika kesi hiyo upande wa mashitaka ulikuwa na mashahidi wanne akiwemo Daktari ambae alithibitisha kuwa msichana huyo alifanyiwa kitendo cha ubakwaji baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kidakitari na kukutwa na mbegu za kiume na upande wa utetezi ulikuwa na mashahidi wanne.

Hakimu mkazi Chiganga Ntengwa baada ya kusikiliza mwenendo mzima wa kesi aliiambia mahakama kuwa mshitakiwa Philipo Emanuel amepatikana na hatia ya kosa la kifungu namba 130 (1)(2) hivyo mahakama inampa nafasi mshitakiwa kabla ya kutolea kwa adhabu kama anayo sababu ya msingi ya kuishawishi mahakama impunguzie adhabu.

Katika utetezi wake mshitaki aliiomba mahakama impunguzie adhabu kwa kuwaanafamilia ya wake wawili ambao wanamtegemea pamoja na watoto ombi ambalo lilipingwa na mwendesha mashitaka.

Baada ya utetezi huo hakimu Chiganga alisoma hukumu kwa kueleza kuwa kutokana na mshitakiwa Emanuel Philipo kupatikana na kosa hilo mahakama imemuhukumu kwenda jela kutumikia kifungo cha miaka 30 jela kuanzia mei 26 mwaka huu.

Chanzo: Katavi yetu