WACHIMBA MGODI 157 WAFA MGODINI

Mlipuko katika mgodi wa makaa ya mawe magharibi mwa Uturuki umesababisha vifo vya zaidi ya wachimbaji migodi 150 na kujeruhi wengine zaidi ya 70 kwa mujibu wa maafisa nchini humo.


Meya wa eneo la Manisa, Cengiz Ergun, ametoa tahadhari kwamba idadi ya watu waliokufa bado haijathibitishwa rasmi.

Inahofiwa kuwa wachimbaji mgodi wengine wengi bado wamefukiwa chini ya mgodi huo.


Inakadiriwa kuwa wakati mlipuko huo ulipotokea wafanyikazi 580 walikuwa ndani ya mgodi huo japo inaaminika wengi waliweza kukimbilia usalama wao.

Bado idadi ya walionaswa ndani ya mgodi huo haijabainika.


Mgodi huo uko katika mji wa Soma, mkoani Manisa , takriban kilomita 250 kusini mwa Istanbul.

Jamaa za wachimbaji migodi hao wamekusanyika katika makundi karibu na mgodi huoambao unamilikiwa na wawekezaji wa kibinafsi hukuwengi wao wakilia hadharani na kububujikwa na machozi.


Waziri wa nishati Taner Yildiz ameimabia televisheni ya Uturuki kuwa huenda wengi wamekufa kutokana na sumuya gesi aina ya carbon monoxide.

Amesema moto huo umesababishwa na hitilafu ya umeme.


Picha za televisheni zinaonyesha maafisa wa uokoaji wakiokoa wafanyikaziwa mgodi huo, huku nyuso zao zao zikiwa zimejaa vumbi.

Baadhi yao wanaweza kutembea na wengine wanabebwa na kupelekwa ndani ya magari ya kubebea wagonjwa yaliyoegezwa karibu na eneo la tukio.