CASTER SEMENYA AMPOSA MWANAMKE MWENZAKE

Habari zimeenea nchini Afrika kusini kwamba Mwanariadha maarufu wa kike nchini humo Caster Semenya amejipatia mchumba wa kike.

Taarifa katika vyombo vya habari nchini humo zinasema kuwa mahari au lobola kama inavyojulikana Afrika kusini imepelekwa kwa familia ya mchumba huyo iliyoko Polokwane jimbo la Limpopo na zikakubaliwa kwa mikono miwilina wazazi wa Violet Raseboya.


Caster Semenya

Kama unanijua vizuri basi unafahamu kuwa Caster hatangamani na vyombo vya habari. Nakutana na waandishi wahabari wakati wa mashindano tu! Na wala sitajishugulisha kujibu kama madai hayo ni kweli au la maanake ni swala ambalo limechapishwa magazetini siwezi kubadili lolote!"

Aidha Lobola yaani mahari ya rand elfu 25 sawa na dola 2500 za Marekani ilikubaliwa kwa mikono miwili.

Hata hivyo Semenya mwenyewe anavilaumu vyombo vya habari kwa kuingilia maisha yake ya kibinafsi.


Mwandishi wa idhaa ya Kiswahili ya BBC nchini Afrika Kusini alipomtaka kuthibitisha kama taarifa hizo ni za ukweli, Semenya alisema hatapinga au kukubali Vyombo vya habari nchini A-Kusini tayari vimeripoti kuwa Caster Semenya (23 ) amekua na uhusiano wa kimapenzi kwa muda sasa na mwanariadha mwenzie wa kike Violet Raseboya.

Mwanariadha huyo aliyegonga vichwa vya habari kote duniani mwaka wa 2009 alipompiku Janeth Jepkosgey wa Kenya na kutwaa ubingwa wa dunia wa mbio za mita 800 za wanawake huko Berlin.


Wakenya walikata rufaa wakitilia shaka jinsia yake kutokana na maumbile yake yenye miraba minne.

Na matukio yaliyofwatia yalimlazimu Semenya kufanyiwa uchunguzi wa siha na jinsia na shirikisho la riadha duniani IAAF jambo lililompa fedheha sana bingwa huyo wa dunia.


Aliporejea nyumbani viongozi walioshabikia ushindi wake walimsifu kuwa binti wa Afrika Kusini na hata magazeti ya urembo ya kachapisha picha zake akiwa amejipodoa.

Mwaka wa 2006 wakati wa utawala wa Thabo Mbeki serikali ya Afrika Kusini ilipitisha sheria ya kuhalalisha mapenzi ya jinsia moja.