BIBI ALIYEKAMATWA NA UNGA APANDISHWA KIZIMBANI

Hatimaye 'Bibi wa unga' raia wa Nigeria, Olabis IbidunCole (65), amepandishwa kizimbanina kusomewa shtaka linalomkabili kwa lugha ya Kiingereza.

Juzi, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliahirisha kesi hiyo hadi jana kwa kile kilichoelezwa kuwa mtuhumiwa hafahamu lugha ya Kiingereza baada ya kusema anafahamu lugha ya Kiyoruba tu.

Hata hivyo, ilielezwa kuwa baada yauchunguzi, ilibainika kuwa alipokamatwa Uwanja wa Ndege waJulius Nyerere, alihojiwa kwa Kiingereza hivyo Mahakama ikamlazimisha kuendelea na lugha hiyo.

"Uchunguzi ulifanywa na mahakam aumebaini kuwa mshtakiwa unafahamu vizuri lugha ya Kiingereza hivyo, kutokana na hili tunakusomea hati yako ya mashtaka kwa lugha ya Kiingereza,"Hakimu wa Mahakama hiyo, Frank Moshi alisema.

Bibi huyo ambaye ni mfanyabiashara na mkazi wa Lagos,Nigeria, alikubali kusomewa hati hiyo kwa lugha ya Kiingereza.

Akisoma hati ya mashtaka, Mwendesha Mashtaka, Mkaguzi wa Polisi, Jackson Chidunda alidai kuwa Cole alikutwa na gramu 831 za dawa za kulevya aina ya heroini zenye thamani ya Sh37 milioni Mei 19, mwaka huu katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere saa tisa jioni.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, Hakimu Moshi alimwambia mshtakiwa kuwa hatakiwi kujibu chochote mahakamani hapo kutokana shtaka linalomkabili kutokuwa na dhamana na aliahirisha kesi hiyo hadi Juni 10, mwaka huu itakapotajwa tena.

Mshtakiwa ambaye anayeshikilia rekodi ya kuwa mtuhumiwa wa dawa za kulevya mwanamke mwenye umri mkubwa kukamatwa kwenye uwanja huo alinaswa alipokuwa akijiandaa kwenda Paris, Ufaransa kwa ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia.


Chanzo: Mwananchi