BABA AMUUA MWANAE WA KIKE KWA MAWE

Mwanamke mmoja nchini Pakistan amepigwa mawe na familia yake wakiwemo babake na ndugu zake wa kiume hadi kufariki. Aliuawa nje ya jengo la mahakama mjini Lahore.

Mwanamke huyo aliuawa kwa kuolewa na mtu ambaye alikuwa chaguo lake mwenyewe.

Farzana Bibi, mwenye umri wa miaka 31, aliolewa na Muhammad Iqbal miezi michache iliyopita bila ya idhini ya familia yake.

Polisi wanasema kuwa mwanamke huyo alishambuliwa na familia yake.

Kaka zake na binamu yake mmoja walimshika alipokuwaakiingia mahakamani na kuanza kumpiga kwa mawe. Alifariki papo hapo.

Waliomuua walikimbia kabla ya polisi kufika katika eneo hilo.

Babake msichana huyo amekamatwa ingawa washukiwa wengine wangali hawajulikani waliko.

Kwa wanawake wanaoolewa na wapenzi ambao ni chaguo lao wenyewe, ni kitendo kisichokubalika kitamaduni katika baadhi ya maeneo ya Pakistan.

Mamia ya wasichana huuawakwa kisingizio cha kuolewa nawatu wasiokubalika na familia zao kila mwaka

Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu, wanaaminikuwa kwa kuwa mauaji hayo hufanywa na familia zenyewe, huwa ni vigumu kufikisha kesi hizo kortini.